< Yohana 12 >

1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
Then Jesus, six days before the passover, came to Bethany, where Lazarus was who had been dead, whom he raised from the dead.
2 Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
There they made him a supper; and Martha served: but Lazarus was one of them that sat at the table with him.
3 Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
Then Mary took a pound of ointment of spikenard, very costly, and anointed the feet of Jesus, and wiped his feet with her hair: and the house was filled with the odor of the ointment.
4 Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
Then saith one of his disciples, Judas Iscariot, Simon's [son], who was to betray him,
5 “Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
Why was not this ointment sold for three hundred pence, and given to the poor?
6 Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
This he said, not that he cared for the poor; but because he was a thief, and had the bag, and bore what was put in it.
7 Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Then said Jesus, Let her alone: against the day of my burial hath she kept this.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
For the poor ye have always with you; but me ye have not always.
9 Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
Many people of the Jews therefore knew that he was there: and they came, not for Jesus' sake only, but that they might see Lazarus also, whom he had raised from the dead.
10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
But the chief priests consulted that they might put Lazarus also to death;
11 kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
Because that by reason of him many of the Jews went away, and believed on Jesus.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
On the next day, many people that had come to the feast, when they heard that Jesus was coming to Jerusalem,
13 Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
Took branches of palm-trees, and went forth to meet him, and cried, Hosanna; Blessed [is] the King of Israel that cometh in the name of the Lord.
14 Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
And Jesus, when he had found a young ass, sat thereon; as it is written,
15 “Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
Fear not, daughter of Sion: behold, thy King cometh, sitting on an ass's colt.
16 Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
These things his disciples understood not at the first: but when Jesus was glorified, then they remembered that these things were written concerning him, and [that] they had done these things to him.
17 Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
The people therefore that were with him when he called Lazarus out of his grave, and raised him from the dead, bore testimony.
18 Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
For this cause the people also met him, for that they heard that he had done this miracle.
19 Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
The Pharisees therefore said among themselves, Perceive ye how ye prevail nothing? behold, the world is gone after him.
20 Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
And there were certain Greeks among them, that came to worship at the feast.
21 Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
The same came therefore to Philip, who was of Bethsaida of Galilee, and desired him, saying, Sir, we would see Jesus.
22 Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
Philip cometh and telleth Andrew: and again, Andrew and Philip tell Jesus.
23 Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
And Jesus answered them, saying, The hour is come, that the Son of man should be glorified.
24 Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
Verily, verily, I say to you, Except a corn of wheat fall into the ground and die, it abideth alone: but if it die, it bringeth forth much fruit.
25 Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios g166)
He that loveth his life shall lose it; and he that hateth his life in this world, shall keep it to life eternal. (aiōnios g166)
26 Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
If any man serve me, let him follow me; and where I am, there shall also my servant be: if any man serve me, him will [my] Father honor.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
Now is my soul troubled; and what shall I say? Father, save me from this hour: but for this cause I came to this hour.
28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
Father, glorify thy name. Then came there a voice from heaven, [saying], I have both glorified [it], and will glorify [it] again.
29 Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
The people therefore that stood by, and heard [it], said that it thundered. Others said, An angel spoke to him.
30 Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
Jesus answered and said, This voice came not because of me, but for your sakes.
31 Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
Now is the judgment of this world: now shall the prince of this world be cast out.
32 Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
And I, if I shall be lifted up from the earth, will draw all [men] to me.
33 Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
(This he said, signifying what death he should die.)
34 Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn g165)
The people answered him, We have heard out of the law that Christ abideth for ever: and how sayest thou, The Son of man must be lifted up? Who is this Son of man? (aiōn g165)
35 Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
Then Jesus said to them, Yet a little while is the light with you. Walk while ye have the light, lest darkness come upon you: for he that walketh in darkness knoweth not whither he goeth.
36 Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
While ye have light, believe in the light, that ye may be the children of light. These things spoke Jesus, and departed, and concealed himself from them.
37 Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
But though he had done so many miracles before them, yet they believed not on him:
38 Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
That the saying of Isaiah the prophet might be fulfilled, which he spoke, Lord, who hath believed our report? and to whom hath the arm of the Lord been revealed?
39 Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
Therefore they could not believe, because that Isaiah said again,
40 “Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
He hath blinded their eyes, and hardened their heart; that they should not see with [their] eyes, nor understand with [their] heart, and be converted, and I should heal them.
41 Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
These things said Isaiah, when he saw his glory, and spoke of him.
42 Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
Nevertheless, among the chief rulers also many believed on him; but because of the Pharisees they did not confess [him], lest they should be put out of the synagogue:
43 Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
For they loved the praise of men more than the praise of God.
44 Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
Jesus cried, and said, He that believeth on me, believeth not on me, but on him that sent me:
45 Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
And he that seeth me, seeth him that sent me:
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
I am come a light into the world, that whoever believeth on me should not abide in darkness.
47 “Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
And if any man hear my words, and believe not, I judge him not: for I came not to judge the world, but to save the world.
48 Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
He that rejecteth me, and receiveth not my words, hath one that judgeth him: the word that I have spoken, the same shall judge him in the last day.
49 Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
For I have not spoken from myself; but the Father who sent me, he gave me a commandment, what I should say, and what I should speak.
50 Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios g166)
And I know that his commandment is life everlasting: whatever I speak therefore, even as the Father said to me, so I speak. (aiōnios g166)

< Yohana 12 >