< Yohana 12 >
1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
kum kume nukkun nakwak yabkaka, Yeecu bou betani, fiye Lizaru wiyeu wo Yeecu fulouweu
2 Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
cin macinen cariwi, matta nima carike, Liazaru wi mor nubo yimwiyeu kange Yeecu.
3 Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
dila matta tuwango ficangeu ciyweki nad, ci belti Yeecu ninti nacek. laci wauki yiri duwecek. mor luweu dimki kundo ficang ficangeu.
4 Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
Yafuda kari yoti wiin mor nob bwankaceb niwo ane konco fiyeu, yiki,
5 “Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
yebwe mani miyeu nuwango ficang ficangeti nai kwinikwo ta'arti naneken nubo manki dikere?
6 Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
citok kero wo nobkici cwinubo manki dikereti, wori cin nikuye: cociyo kemerotiye, takri kudike ciyokangce keti.
7 Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Yeecu yiki, dobco ciya yoken dike cidou na fwekami koceu
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
kwatti kom wari kange nob bwinibi, kommani wari kange mo.”
9 Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
kambo Yafudawa ducce nyumom Yeecu wini yeri la cin bou, kebo Yeecu nin ki kwace, cibou nacin to Liazaru, wo Yeecu fulou buwareu.
10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
la liya wabetin do dou nuriti ciya twalum Liayazaru ti kencu,
11 kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
inkercen Yafudawa ducce yane bilnike Yeecu nine.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
celfiniceri namor ka nubeko ducce cin bou fiye Idii. kaci nuwa ker Yeecu bouti wurcalima,
13 Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
la cin yeu bilu dibin cin ceru'u cin ker co dila cin kun diro citi toki Hosana; be buyer kiniwo bou kiden kwamareu, liya Yafudawa.”
14 Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
Yeecu fiyaube Gelban kwiken dorcer kambo bulangeu,
15 “Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
cwaretai mo cihiyona, to liya kume bouti yimdor gelbar.”
16 Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
nob bwankan cebo yombo dikowo kikabe, kambo ci duklang Yeecuri, la cin kwabidikewo mulangi nyo dor Yeecur, la cin ma cinen dikerowo.
17 Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
la nubowo wari kange Yeecu ki kumewo ci cuwo Liyazaru mor tuwe cin fuloucou, cinen bilenke.
18 Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
wonco dike bwi nubo cirou yaercou, wori ciin nuwa cin ma dikewo.
19 Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
la Firicawa yoten kero bwiti ki, “to mani ka ma dike kangeti, komto dorbitinero bwangtenco.
20 Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
morece Helinawa wi birombo yakentiwi fiye wabka Idii.
21 Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
cin yaken Filibu nin, inni becaida yim Galili, “cii ki, nii merangka, nyin cwiti nyin to Yeecu.
22 Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
Filibu yanyi Andirawu yaken wari kange Filibu yacin yi Yeecu.
23 Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
Yeecu ciya yicii, kang keno ko din wo ciya ne bibwe nii duktang tiye.
24 Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
bilenke, bilenke, miyikomti, la nu'u bikateu an yarken bitine na buyam, cannowi cike kwaco, cano cibuyamri, canne bituttitui.
25 Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios )
niwo cwi dume cetiyeu, an lomco lano ko dumece kalereri atin yoken co dume wo diri diriyeu. (aiōnios )
26 Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
ni wo wabyetiyeri, la abwang menten. fiye miwiyeu. bwe can nya miu anowinken. niwo wabyeti yeri, kwama an neco duri.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
naweu dume mi kino mor kwomka, yemama tiye? tee cokye ki kwama wo? wonco dike bwi milau kwama.
28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
tee, duktang den mwero “la diro yirau di kwama ki, min duktangce, man duktangcotak.
29 Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
la nyori nubo murom wiyeu nuwa diro, cin yi ki kwama kwabi. kanyembo ki nii tomangeu tokker kange co.”
30 Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
Yeecu ciya ci ki, dirowo boubo minen, bou kumen.
31 Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
naweu ciyatin warkaleu: na weu atin ywa nii liyar kalero.
32 Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
na nyime mo, canno cii kunye dorbitinerdi, man bou ki nubo kwareub fiye mwiyeu”
33 Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
ci tokwo nadong dara buwareu ca bwiya tiyeu.
34 Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn )
nubo ciyaco yiki, nyin nuwa mor werfuner kiritti a yi nyo diri. ye bwi mutok muki atin kun bibweni ye? we bibweni ciro? (aiōn )
35 Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
Yeecu inyici, “kakten biduwardi kam yi ki filang kamyi kange filango ki kwama wo filango wari kange komeu, ka kumtacileu cumomkom. wo yam mor kumtacileu, nyombo fiye ciyakenti wiyeu.
36 Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
komne bilenke filanko wonin kambo kom wari kange filange nakom yilam bebei filang. Yeecu tokwori colem ya Yuranngum me.
37 Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
cano Yeecu inma diker nyiman kar ducce kabumcim. kwarub kange wo, cinebo bilinki anen.
38 Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
naker dukumer Icayarodin, woki, kwama, we nebilinke ker nyere? kang kwama ko bou wenin?”
39 Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
wonco dike bwi ci nebo bilinker, Icaya toktentak,
40 “Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
cin cumom nuweceu, cin kwamum nerciro, wore na ci tore ki nuwece, naci nyomde ki nercer, yilau minen nan nirimci.
41 Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
Icaya tok kerowo inwori cinto duktanka Yeecu kon tok ker kangeco.
42 Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
nawo duwoleu, ducce mor duremcin nin nebilinke Yeecu nin dila Faricawa, ci dambo yomka ceko dangla.
43 Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
cin cwi caklangka la caklangka ko bou kwama ninneu.
44 Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
Yeecu kung diro yiki, niwo bilenke mi nen neure keboka minen cine bilenke kange niwo two mu yerou,
45 Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
niwo to yereu, tom niwo two mu yereu.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
me bou nan filang dor bitiner, canowo nebitinke minendi mani yiti mor kumtacile.
47 “Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
ni wo nuwa kermiro nebo bilenkeri, mani maci nen bolangti, mi bou bo nan ma dor bitinero nin bolang, bi bou nan fulo dor bitinero.
48 Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
niwo keya, koten kermireu, niwo a maci nen bolangko tiyeu wi kero matokeu an maci nen bolang ki kume cwile.
49 Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
ma tokbo ker doret mer inker teero twomu yereu, niwo yiye dike ma matiyeu kange dike matok tiyeu.
50 Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios )
min nyimom nyalcero nawo diriye, co dike bwe matoke-nawo tee tokeu, nyo matoke.” (aiōnios )