< Yohana 11 >
1 Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
Agora um certo homem estava doente, Lázaro de Betânia, da aldeia de Maria e sua irmã, Marta.
2 Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
Era aquela Maria que havia ungido o Senhor com pomada e limpado seus pés com seus cabelos, cujo irmão Lázaro estava doente.
3 Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
As irmãs, portanto, enviaram a ele, dizendo: “Senhor, eis que aquele por quem tu tens grande afeição está doente”.
4 Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
Mas quando Jesus ouviu isso, disse: “Esta doença não é para a morte, mas para a glória de Deus, para que o Filho de Deus seja glorificado por ela”.
5 Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
Agora Jesus amava Marta, e sua irmã, e Lázaro.
6 baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
Quando ouviu que estava doente, ficou dois dias no lugar onde estava.
7 Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
Depois disso, ele disse aos discípulos: “Vamos para a Judéia novamente”.
8 Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
Os discípulos lhe perguntaram: “Rabino, os judeus estavam apenas tentando apedrejá-lo. Você vai lá novamente”?
9 Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
Jesus respondeu: “Não há doze horas de luz do dia? Se um homem caminha no dia, ele não tropeça, porque vê a luz deste mundo.
10 Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
Mas se um homem caminha de noite, ele tropeça, porque a luz não está dentro dele”.
11 Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
Ele disse estas coisas, e depois disso, disse-lhes: “Nosso amigo Lázaro adormeceu, mas eu vou para que eu possa despertá-lo do sono”.
12 Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
Portanto, os discípulos disseram: “Senhor, se ele adormeceu, ele se recuperará”.
13 Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
Agora Jesus havia falado de sua morte, mas eles pensavam que ele falava em descansar durante o sono.
14 Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
Então Jesus lhes disse claramente: “Lázaro está morto”.
15 Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
Fico feliz por vocês que eu não estava lá, para que vocês possam acreditar. No entanto, vamos até ele”.
16 Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
Tomé, portanto, que se chama Didymus, disse a seus companheiros discípulos: “Vamos também, para que possamos morrer com ele”.
17 Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
Então, quando Jesus chegou, descobriu que já havia estado no túmulo quatro dias.
18 Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
Agora Betânia estava perto de Jerusalém, a cerca de quinze estádios de distância.
19 na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
Muitos dos judeus tinham se unido às mulheres ao redor de Marta e Maria, para consolá-las a respeito de seu irmão.
20 Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
Então, quando Marta soube que Jesus estava chegando, foi ao seu encontro, mas Maria ficou na casa.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
Por isso Marta disse a Jesus: “Senhor, se você estivesse aqui, meu irmão não teria morrido”.
22 Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
Mesmo agora eu sei que tudo o que você pedir a Deus, Deus lhe dará”.
23 Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
Jesus lhe disse: “Seu irmão ressuscitará”.
24 Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
Martha disse-lhe: “Eu sei que ele ressuscitará na ressurreição no último dia”.
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
Jesus lhe disse: “Eu sou a ressurreição e a vida”. Aquele que acredita em mim ainda viverá, mesmo que morra”.
26 na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn )
Quem vive e acredita em mim, jamais morrerá. Você acredita nisto”? (aiōn )
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
Ela disse a ele: “Sim, Senhor”. Eu vim a acreditar que você é o Cristo, o Filho de Deus, aquele que vem ao mundo”.
28 Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
Quando ela disse isto, foi embora e chamou Maria, sua irmã, secretamente, dizendo: “O Professor está aqui e está chamando você”.
29 Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
Ao ouvir isso, ela se levantou rapidamente e foi até ele.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
Agora Jesus ainda não tinha entrado na aldeia, mas estava no lugar onde Marta o encontrou.
31 Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
Então os judeus que estavam com ela em casa e a consolavam, quando viram Maria, que ela se levantou rapidamente e saiu, a seguir, dizendo: “Ela está indo para o túmulo para chorar lá”.
32 Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
Portanto, quando Maria chegou onde Jesus estava e o viu, caiu a seus pés, dizendo-lhe: “Senhor, se tu estivesses aqui, meu irmão não teria morrido”.
33 Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
Portanto, quando Jesus a viu chorar, e os judeus chorando quem veio com ela, ele gemeu no espírito e ficou perturbado,
34 Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
e disse: “Onde você o colocou? Disseram-lhe: “Senhor, vem e vê”.
36 Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
Portanto, os judeus disseram: “Veja quanto carinho ele tinha por ele”!
37 Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
Alguns deles disseram: “Não poderia este homem, que abriu os olhos dele que era cego, também ter impedido que este homem morresse?”
38 Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
Jesus, portanto, novamente gemendo em si mesmo, veio ao túmulo. Agora era uma caverna, e uma pedra estava contra ela.
39 Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
Jesus disse: “Tirai a pedra”. Martha, a irmã dele que estava morta, disse-lhe: “Senhor, por esta altura já há um fedor, pois ele está morto há quatro dias”.
40 Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
Jesus lhe disse: “Eu não lhe disse que se você acreditasse, você veria a glória de Deus”?
41 Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
Então eles tiraram a pedra do lugar onde o morto estava deitado. Jesus levantou os olhos e disse: “Pai, eu te agradeço por me teres ouvido.
42 Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
Eu sei que você sempre me escuta, mas por causa da multidão ao redor eu disse isto, para que eles possam acreditar que você me enviou”.
43 Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
Quando ele disse isto, gritou com voz alta: “Lázaro, sai daí!”.
44 Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
Aquele que estava morto saiu, amarrou a mão e o pé com envoltórios, e seu rosto foi enrolado com um pano. Jesus disse-lhes: “Libertai-o e deixai-o ir”.
45 Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
Portanto, muitos dos judeus que vieram a Maria e viram o que Jesus acreditava nele.
46 Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
Mas alguns deles foram até os fariseus e lhes contaram as coisas que Jesus havia feito.
47 Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
Portanto, os chefes dos sacerdotes e os fariseus reuniram um conselho, e disseram: “O que estamos fazendo? Pois este homem faz muitos sinais.
48 Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
Se o deixarmos assim sozinho, todos acreditarão nele, e os romanos virão e tirarão tanto nosso lugar quanto nossa nação”.
49 Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
Mas um certo Caifás, sendo sumo sacerdote naquele ano, disse-lhes: “Vocês não sabem nada,
50 Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
nem consideram que é vantajoso para nós que um homem morra pelo povo, e que a nação inteira não pereça”.
51 Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
Agora ele não disse isto de si mesmo, mas sendo sumo sacerdote naquele ano, profetizou que Jesus morreria pela nação,
52 wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
e não somente pela nação, mas que ele também poderia reunir em um só os filhos de Deus que estão espalhados no exterior.
53 Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
Assim, a partir daquele dia, eles tomaram conselhos para que o pudessem condenar à morte.
54 Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
Portanto, Jesus não andou mais abertamente entre os judeus, mas partiu dali para o campo perto do deserto, para uma cidade chamada Efraim. Ele ficou lá com seus discípulos.
55 Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
Agora a Páscoa dos judeus estava à mão. Muitos subiram do país para Jerusalém antes da Páscoa, para se purificarem.
56 Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
Então procuraram por Jesus e falaram uns com os outros enquanto estavam no templo: “O que você acha - que ele não vem à festa de modo algum”?
57 Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.
Agora os chefes dos sacerdotes e os fariseus tinham ordenado que, se alguém soubesse onde ele estava, o informasse, para que eles o apreendessem.