< Yohana 11 >
1 Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
Il y avait un malade, Lazare, de Béthanie, village de Marie et de Marthe, sa sœur.
2 Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
— Marie est celle qui oignit de parfum le Seigneur, et lui essuya les pieds avec ses cheveux; et c’était son frère Lazare qui était malade. —
3 Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
Les sœurs envoyèrent dire à Jésus: « Seigneur, celui que vous aimez est malade. »
4 Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
Ce qu’ayant entendu, Jésus dit: « Cette maladie ne va pas à la mort, mais elle est pour la gloire de Dieu, afin que le Fils de Dieu soit glorifié par elle. »
5 Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
Or, Jésus aimait Marthe, et sa sœur Marie, et Lazare.
6 baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
Ayant donc appris qu’il était malade, il resta deux jours encore au lieu où il était.
7 Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
Il dit ensuite à ses disciples: « Retournons en Judée. »
8 Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
Les disciples lui dirent: « Maître, tout à l’heure les Juifs voulaient vous lapider, et vous retournez là? »
9 Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
Jésus répondit: « N’y a-t-il pas douze heures dans le jour? Si quelqu’un marche pendant le jour, il ne se heurte point, parce qu’il voit la lumière de ce monde.
10 Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
Mais s’il marche pendant la nuit, il se heurte, parce qu’il manque de lumière. »
11 Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
Il parla ainsi, et ajouta: « Notre ami Lazare dort, mais je me mets en route pour le réveiller. »
12 Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
Ses disciples lui dirent: « S’il dort, il guérira. »
13 Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
Mais Jésus avait parlé de sa mort, et ils pensaient que c’était du repos du sommeil.
14 Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
Alors Jésus leur dit clairement: « Lazare est mort;
15 Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
et je me réjouis à cause de vous de n’avoir pas été là, afin que vous croyiez; mais allons vers lui. »
16 Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
Et Thomas, appelé Didyme, dit aux autres disciples: « Allons-y, nous aussi, afin de mourir avec lui. »
17 Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
Jésus vint donc et trouva Lazare depuis quatre jours dans le sépulcre.
18 Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
Or Béthanie était près de Jérusalem, à quinze stades environ.
19 na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
Beaucoup de Juifs étaient venus près de Marthe et de Marie pour les consoler au sujet de leur frère.
20 Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
Dès que Marthe eut appris que Jésus arrivait, elle alla au-devant de lui, tandis que Marie se tenait assise à la maison.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
Marthe dit donc à Jésus: « Seigneur, si vous aviez été ici, mon frère ne serait pas mort.
22 Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
Mais maintenant encore, je sais que tout ce que vous demanderez à Dieu, Dieu vous l’accordera. »
23 Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
Jésus lui dit: « Votre frère ressuscitera. —
24 Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
Je sais, lui répondit Marthe, qu’il ressuscitera lors de la résurrection, au dernier jour. »
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
Jésus lui dit: « Je suis la résurrection et la vie; celui qui croit en moi, fût-il mort, vivra;
26 na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn )
et quiconque vit et croit en moi, ne mourra point pour toujours. Le croyez-vous? — (aiōn )
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
Oui, Seigneur, lui dit-elle, je crois que vous êtes le Christ, le Fils de Dieu, qui devait venir en ce monde. »
28 Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
Lorsqu’elle eut ainsi parlé, elle s’en alla, et appela en secret Marie, sa sœur, disant: « Le Maître est là, et il t’appelle. »
29 Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
Dès que celle-ci l’eut entendu, elle se leva promptement et alla vers lui.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
Car Jésus n’était pas encore entré dans le village; il n’avait pas quitté le lieu où Marthe l’avait rencontré.
31 Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
Les Juifs qui étaient avec Marie, et la consolaient, l’ayant vue se lever en hâte et sortir, la suivirent en pensant: « Elle va au sépulcre pour y pleurer. »
32 Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
Lorsque Marie fut arrivée au lieu où était Jésus, le voyant, elle tomba à ses pieds, et lui dit: « Seigneur, si vous aviez été ici, mon frère ne serait pas mort. »
33 Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
Jésus la voyant pleurer, elle et les Juifs qui l’accompagnaient, frémit en son esprit, et se laissa aller à son émotion.
34 Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
Et il dit: « Où l’avez-vous mis? — Seigneur, lui répondirent-ils, venez et voyez. »
36 Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
Les Juifs dirent: « Voyez comme il l’aimait! »
37 Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
Mais quelques-uns d’entre eux dirent: « Ne pouvait-il pas, lui qui a ouvert les yeux d’un aveugle-né, faire aussi que cet homme ne mourût point? »
38 Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
Jésus donc, frémissant de nouveau en lui-même, se rendit au sépulcre: c’était un caveau, et une pierre était posée dessus.
39 Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
« Ôtez la pierre », dit Jésus. Marthe, la sœur de celui qui était mort, lui dit: « Seigneur, il sent déjà, car il y a quatre jours qu’il est là. »
40 Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
Jésus lui dit: « Ne vous ai-je pas dit que si vous croyez, vous verrez la gloire de Dieu? »
41 Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
Ils ôtèrent donc la pierre; et Jésus leva les yeux en haut et dit: « Père, je vous rends grâces de ce que vous m’avez exaucé.
42 Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
Pour moi, je savais que vous m’exaucez toujours; mais j’ai dit cela à cause de la foule qui m’entoure, afin qu’ils croient que c’est vous qui m’avez envoyé. »
43 Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
Ayant parlé ainsi, il cria d’une voix forte: « Lazare, sors! »
44 Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
Et le mort sortit, les pieds et les mains liés de bandelettes, et le visage enveloppé d’un suaire. Jésus leur dit: « Déliez-le, et laissez-le aller. »
45 Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
Beaucoup d’entre les Juifs qui étaient venus près de Marie et de Marthe, et qui avaient vu ce qu’avait fait Jésus, crurent en lui.
46 Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
Mais quelques-uns d’entre eux allèrent trouver les Pharisiens, et leur racontèrent ce que Jésus avait fait.
47 Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
Les Pontifes et les Pharisiens assemblèrent donc le Sanhédrin et dirent: « Que ferons-nous? Car cet homme opère beaucoup de miracles.
48 Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
Si nous le laissons faire, tous croiront en lui, et les Romains viendront détruire notre ville et notre nation. »
49 Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
L’un d’eux, Caïphe, qui était grand prêtre cette année-là, leur dit: « Vous n’y entendez rien;
50 Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
vous ne réfléchissez pas qu’il est de votre intérêt qu’un seul homme meure pour le peuple, et que toute la nation ne périsse pas. »
51 Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
Il ne dit pas cela de lui-même; mais étant grand prêtre cette année-là, il prophétisa que Jésus devait mourir pour la nation; —
52 wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
et non seulement pour la nation, mais aussi afin de réunir en un seul corps les enfants de Dieu qui sont dispersés.
53 Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
Depuis ce jour, ils délibérèrent sur les moyens de le faire mourir.
54 Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
C’est pourquoi Jésus ne se montrait plus en public parmi les Juifs; mais il se retira dans la contrée voisine du désert, dans une ville nommée Ephrem, et il y séjourna avec ses disciples.
55 Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
Cependant la Pâque des Juifs était proche, et beaucoup montèrent de cette contrée à Jérusalem, avant la Pâque, pour se purifier.
56 Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
Ils cherchaient Jésus et ils se disaient les uns aux autres, se tenant dans le temple: « Que vous en semble? Pensez-vous qu’il ne viendra pas à la fête? »
57 Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.
Or, les Pontifes et les Pharisiens avaient donné l’ordre que, si quelqu’un savait où il était, il le déclarât, afin qu’ils le fissent prendre.