< Yohana 10 >
1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
Etesheli, Etesheli embabhozya, ola wasahwinjila ashilile mundyango gwi goma lye ngole, ila azubha hwidala lya mwabho, omuntu oyo mwibha na fyozi.
2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
Omwane wa hwinjila mundyango yodimi we ngole.
3 Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
Hwa mweme olinzi we dyango ahwigulilwa. Engolezolyonvwa izu lyakwe na azikwi zya engole zyakwe hu matawa gabho na zifumye honze.
4 Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
Naizifumya honze ezye zyazili zyakwe azitangulila ne Ngolobhe zihulondolela, afuatanaje bhalimenye izu lyakwe.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
Sezinzahumwanze ojenyu ila zinza hupemushile, afuatane sezigamenye amazu ga jenyu.”
6 Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
O Yesu ayanga ofwana ogu hwabhene, ila sebhazyelewe enongo ezi zyali ayanag hwa bhene.
7 Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
O Yesu ayanga nabho nantele, “Etesheli, etesheli, embabhozya, Ane endi ndiango gwe ngole.
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
Bhonti bhabhatanguliye bhibha na bhafyozi, ila engole zibhonvwa.
9 Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
Ane endi ndiango. Wawonti wahwinjila ashilile huline, aifyoliwa ainjila muhati na fume, wope aipata edyo.
10 Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
Omwibha sahwenza ila ahwibhe, agoje, natezye, enenzele nkawepate owomi bhabhe nawo winji.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Ane endi dimi mwinza. Odimi omwinza afumya owomi wakwe huu ngole.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
Oboyi wabhehwelwe, nasio aje dimi, ola engole se vyoma vyakwe, azilola embwa zihwenza na azileha na zishembele.
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
Ne mbwa zikhata na nyampanye. Zishembela afuatanaji oboyi wabhe hwelwe sazisajila engole.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua.
Ane endi dimi mwinza embamenye bhabhali bhahuline, wope wamenye ane.
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
Odaada amenye, nane emenye Odaada, nane eufumwa owomi wane hungole.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili, inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu, hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
Endi nazyo engole zimo zyasaga zya mwigoma eli ezyo zyope ehwanziwa azilete, zyope zinzahonvwe izu lyane zibheligoma limo no dimi omo.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
Ene ndiyo maana Odaada angene: Eeufumye owomi wane alafu nantele aweje.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
Nomo wawega afume huline, ila eufumya nene. Endi waamuzi gwa ufumye na endi waamuzi ogwagwefwe nantele. Endiposheye elajizyo eli afume hwa Daada.”
19 Kwa maneno haya Wayahudi waligawanyika.
Olwaganyishe lwafuma afume hwa yahudi afuatana na maazu ega.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
Abhinji bhabho wahaga, “Ali ni pepo ndii na pelusu yenu muhumwonvwa?”
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
Bhamo bhayanga, “Ege semazu gamuntu wali ni pepo. Ipepo ligamwigula amaso ompofu?”
22 Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
Nkashahenza Eshikulukulu Shabhehwe Wakifu hu Yelusalemu.
23 Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
Hwali shipindi shi sasa, oYesu ali ajenda mushibhanza muukumbi wa Sulemani.
24 Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
Ayahudi nkabhazyongola na hubhozye, “Paka ndii waibheha nsebho? nkashe awe we Kilisiti, tibhozye peupe.
25 Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
O Yesu ajile, “Embabhozezye ila semuhweteshela. Embombo zyenzibhomba witawa lya Daada wane, ezyo zihakikisha pamwanya yane.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
Ata sheshi ahweteshela alenganaje amwe semuli ngole zyane.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
Engole zyane zihonvwa izu lyane; Enzimenye, zyope zinanza ane.
28 nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn , aiōnios )
Embapiye owomi wewilawila sebhatega na mwaha, nomo hata weka waibhafyola afume mukhono gwane. (aiōn , aiōnios )
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
Odaada wane, wampiye ebho, yo Gosi ashile bhamwabho bhonti, na nomo hata weka wali no uwezo wa fyole mukhono gwa Daada.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
Ane no Daada tili hantu hamo.”
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
Bhanyemla amawe aje nkabhapole nantele.
32 lakini Yesu akawaambia, “Nimewaonyesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni ipi katika hiyo mnataka kunipiga mawe?”
O Yesu abhabhozya, “Embalanjile embombo enyinji enyinza afume hwa Daada. Hu mbombo zyalihu kati yezyo zyamuhwanza ampole na mawe?”
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ingawa ni mwanadamu unajifanya kuwa Mungu.”
Ayahudi bhahaga, “Setihupola na mawe hu mbombo yayonti yeli nyinza, ila okufuru awe wo muntu ohwibheha aje oli Ngolobhe.”
34 Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Sheria ya kwamba, ‘Nimesema kuwa, ninyi ni miungu?’
O Yesu abhabhozya, “Seya handihwe mundajizyo zyenyu, 'Nayanjile, “'Amwe muli mangolobhe'”?”
35 Kama aliwaita ‘miungu,’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
Nkashe abhakwizizye mangolobhe, hwa bhala Izu lya Ngolobhe lya bhenzeye (na Maazu segawezi abudwe),
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’
muyanga ahusu ola Odaada afumizye na husontezye munsi, 'Osalanya,' alengane naje nayanjile, 'ane endi Mwana wa Ngolobhe'?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini,
“Nkashe sebhomba embombo zya Daada wane, mungaje aneteshele.
38 lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ndani yake.”
Ata sheshi, nkashe ezibhomba, ata nkasemuneteshela, zyetesheli embombo aje muwezye amanye na hwelewe aje Odaada ali muhati yane nane muhati ya Daada.”
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
Bhalenga na hu khate oYesu, ahwisogoleye afume mumakhono gabho.
40 Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
O Yesu ahwibhalila hwi syelelye Yordani esehemu hula oYohana hwahozyaga ahwande, ahakhala ohwo.
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
Abhantu abhinji bhahenza hwa Yesu. Bhahendeleye ayanje, “O Yohana lyoli sagabhombile eishara yoyonti, ila enongwa zyonti zyayanjile Yohana ahusu omuntu ono zye yoli.”
42 Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
Abhantu abhinji bhamweteshela oYesu epo.