< Yohana 10 >

1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
”אני אומר לכם באמת, “המשיך ישוע,”מי שמסרב להיכנס למכלאת הצאן דרך השער, ובוחר להיכנס בדרך הצדדית, הוא גנב או שודד.
2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
האדם שנכנס דרך השער הוא רועה הצאן.
3 Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
השומר יפתח לו את השער, עדר הצאן ישמע ויכיר את קולו, והרועה יוביל את הצאן החוצה כשהוא נוקב בשם כל כבשה.
4 Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
הרועה הולך בראש והעדר נוהר אחריו, כי הוא מזהה את הרועה ומכיר את קולו.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
הצאן לא תלכנה אחרי אדם זר, אלא תברחנה מפניו, כי קולו אינו מוכר להן.“
6 Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
אלה ששמעו משל זה מפי ישוע לא הבינו למה התכוון,
7 Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
ולכן ישוע הסביר להם:”אמן אני אומר לכם: אני השער של מכלאת הצאן.
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
כל אלה שבאו לפני היו גנבים ושודדים, אולם הצאן לא שמעו בקולם.
9 Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
כן, אנוכי השער. הנכנסים דרכי יוושעו וימצאו מרעה עשיר בבואם ובצאתם.
10 Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
הגנב בא לגנוב, להרוג ולהשמיד, ואילו אני באתי להעניק חיים בשפע.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
”אני הרועה הטוב, ורועה טוב מקריב את חייו למען צאנו.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
כאשר רועה שכיר יראה זאב מתקרב, הוא יברח ויעזוב את הצאן לאנחות, כי העדר אינו שייך לו, והזאב יחטוף ויפזר את הצאן.
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
הרועה השכיר יברח, משום שאינו אלא שכיר ואין הוא דואג לצאן באמת.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua.
”אני הרועה הטוב; אני מכיר את צאני והן מכירות אותי,
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
כשם שאבי מכיר אותי ואני מכיר את אבי; ואני מקריב את חיי למען הצאן.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili, inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu, hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
יש לי עדר נוסף שאינו מהמכלאה הזאת. עלי להנהיג גם אותו, והצאן שומעות בקולי; כך יהיה עדר אחד ורועה אחד.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
”אבי אוהב אותי משום שאני מקריב את חיי כדי שאקבל אותם חזרה.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
איש אינו יכול להרוג אותי ללא הסכמתי. אני מקריב את חיי מרצוני, מפני שיש לי זכות וכוח להקריב את חיי כשאני רוצה בכך, ואף זכות וכוח להשיבם לעצמי. אלוהים הוא המעניק לי זכות זאת.“
19 Kwa maneno haya Wayahudi waligawanyika.
דבריו אלה שוב גרמו למחלוקת בין מנהיגי היהודים.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
חלקם אמר:”או שהוא יצא מדעתו, או שנכנס בו שד! מדוע אתם מקשיבים לו?“
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
אחרים אמרו:”הוא אינו נשמע כמי שנכנס בו שד. האם שד יכול לפקוח עיני עיוורים?“
22 Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
בחג החנוכה, בחורף,
23 Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
התהלך ישוע בבית־המקדש באגף הנקרא”אולם שלמה“.
24 Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
היהודים הקיפוהו מכל עבר ושאלו:”עד מתי בכוונתך לסקרן אותנו? אם אתה הוא המשיח, מדוע אינך אומר זאת בפירוש?“
25 Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
”כבר אמרתי לכם, אבל לא האמנתם לי“, השיב ישוע.”המעשים שאני עושה בשם אבי מאשרים זאת.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
אולם אינכם מאמינים לי, כי אינכם שייכים לצאני.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
אני מכיר את צאני, צאני מכירות את קולי והן הולכות אחרי.
28 nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn g165, aiōnios g166)
אני מעניק להן חיי נצח והן לא תאבדנה. איש לא יחטוף אותן ממני, (aiōn g165, aiōnios g166)
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
כי אבי נתן לי אותן, והוא חזק וגיבור מכולם. משום כך לא יוכל איש לחטוף אותן ממני.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
אבי ואני אחד אנחנו!“
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
שוב החלו מנהיגי היהודים להשליך עליו אבנים.
32 lakini Yesu akawaambia, “Nimewaonyesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni ipi katika hiyo mnataka kunipiga mawe?”
”הראיתי לכם הרבה מעשים טובים בשם אבי, איזה מהם גרם לכך שתשליכו עלי אבנים?“שאל ישוע.
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ingawa ni mwanadamu unajifanya kuwa Mungu.”
”איננו משליכים עליך אבנים בגלל המעשים הטובים שעשית, אלא בגלל שאתה מגדף את האלוהים; למרות שאתה אדם, אתה עושה את עצמך לאלוהים!“
34 Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Sheria ya kwamba, ‘Nimesema kuwa, ninyi ni miungu?’
”אך הכתובים שלכם אומרים:’אלוהים אתם‘, והכוונה היא לבני־האדם“, השיב ישוע.
35 Kama aliwaita ‘miungu,’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
”אם האנשים שאליהם מדברים הכתובים מכונים’אלוהים‘, והכתוב הוא דבר אמת,
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’
מדוע קוראים אתם’מגדף‘למי שקדשו האב ונשלח לעולם הזה על־ידו, ושטוען כי הוא בן האלוהים?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini,
אם איני עושה מעשים כפי שעושה אבי, אל תאמינו לי.
38 lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ndani yake.”
אולם אם אני אכן עושה את מעשי אבי, האמינו לפחות למעשים גם אם אינכם מאמינים לי, ואז תשוכנעו שאבי שוכן בי ואני בו.“
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
הם שוב רצו לתפוס את ישוע, אולם הוא התחמק מידיהם.
40 Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
ישוע חזר לעבר הירדן, למקום שבו הטביל יוחנן לראשונה. הוא נשאר שם זמן־מה,
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
ואנשים רבים הלכו אחריו.”יוחנן לא חולל נסים, “אמרו זה לזה,”אולם כל מה שאמר על האיש הזה היה אמת.“
42 Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
אנשים רבים במקום ההוא האמינו כי ישוע באמת המשיח.

< Yohana 10 >