< Yohana 10 >

1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
„Ma räägin teile tõtt: igaüks, kes ei tule lambatarasse värava kaudu, vaid ronib sisse muul moel, on varas ja röövel.
2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
See, kes tuleb sisse värava kaudu, on lammaste karjane.
3 Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
Väravavaht avab talle ja lambad vastavad tema häälele. Ta hüüab oma lambaid nimepidi ja juhib nad välja.
4 Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
Kui ta on nad välja viinud, kõnnib ta nende ees ja lambad järgnevad talle, sest nad tunnevad tema häält.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
Võõrale nad ei järgneks. Õigupoolest põgenevad nad võõra eest, sest nad ei tunne võõraste häält.“
6 Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
Kui Jeesus esitas selle illustratsiooni, siis kuulajad ei mõistnud, mida ta sellega mõtles.
7 Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
Niisiis selgitas Jeesus uuesti: „Ma räägin teile tõtt: mina olen lammaste värav.
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
Kõik, kes tulid enne mind, olid vargad ja röövlid, kuid lambad ei kuulanud neid.
9 Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
Mina olen värav. Igaüks, kes tuleb sisse minu kaudu, saab tervendatud. Nad saavad tulla ja minna ning vajalikku toidust leida.
10 Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
Varas tuleb ainult varastama, tapma ja hävitama. Mina olen tulnud teile tooma elu – elu, mis on pilgeni täis.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Mina olen hea karjane. Hea karjane jätab oma elu lammaste eest.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
Lambaid valvama palgatud inimene ei ole karjane ja ta põgeneb, kui näeb hunti tulemas. Ta jätab lambad maha, sest nad pole tema omad, ning hunt ründab karja ja pillutab selle laiali,
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
sest mees töötab üksnes palga pärast ega hooli lammastest.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua.
Mina olen hea karjane. Mina tunnen omi ja nemad tunnevad mind,
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
just nagu Isa tunneb mind ja mina tunnen teda. Ma jätan oma elu lammaste eest.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili, inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu, hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
Mul on teisi lambaid, kes ei ole selles taras. Ma pean nemadki siia tooma. Nad kuulavad mu häält ja siis on üks kari ühe karjasega.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
Sellepärast Isa armastab mind, et ma jätan oma elu, et saaksin selle jälle võtta.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
Keegi ei võta seda minult; mina otsustasin selle jätta. Mul on õigus see jätta ja õigus see tagasi võtta. See on käsk, mille mu Isa mulle andis.“
19 Kwa maneno haya Wayahudi waligawanyika.
Nende sõnade pärast olid juudid taas Jeesuse suhtes lahkarvamusel.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
Paljud neist ütlesid: „Ta on kurjast vaimust vaevatud! Ta on hullumeelne! Miks te teda kuulate?“
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
Teised ütlesid: „Kurjast vaimust vaevatu ei räägi selliseid sõnu. Pealegi, kuri vaim ei suuda pimedate silmi avada.“
22 Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
Oli talv ja Jeruusalemmas templi pühitsemise püha aeg.
23 Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
Jeesus kõndis templis Saalomoni sammaskäigus. Juudid ümbritsesid teda ja küsisid:
24 Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
„Kui kaua sa hoiad meid teadmatuses? Kui sa oled Messias, siis ütle meile otse!“
25 Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
Jeesus vastas: „Ma juba ütlesin teile, aga te keeldute uskumast. Imeteod, mida ma oma Isa nimel teen, tõendavad, kes ma olen.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
Te ei usu mind, sest te pole minu lambad.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
Minu lambad tunnevad mu häält; ma tunnen neid ja nad järgnevad mulle.
28 nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn g165, aiōnios g166)
Ma annan neile igavese elu; nad ei lähe eales kaotsi ja keegi ei saa neid minult ära kahmata. (aiōn g165, aiōnios g166)
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
Minu Isa, kes nad mulle andis, on kõigist suurem; keegi ei saa neid temalt ära kahmata.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
Mina ja Isa oleme üks.“
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
Taaskord haarasid juudid kivid, et ta kividega surnuks visata.
32 lakini Yesu akawaambia, “Nimewaonyesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni ipi katika hiyo mnataka kunipiga mawe?”
Jeesus ütles neile: „Te olete näinud palju häid tegusid, mida ma olen Isalt teinud. Millise eest neist te mind kividega viskate?“
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ingawa ni mwanadamu unajifanya kuwa Mungu.”
Juudid vastasid: „Me ei viska sind kividega hea tegemise pärast, vaid jumalateotuse pärast, sest sa oled kõigest inimene, kuid väidad, et oled Jumal.“
34 Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Sheria ya kwamba, ‘Nimesema kuwa, ninyi ni miungu?’
Jeesus vastas neile: „Kas teie seaduses pole kirjutatud: „Ma ütlesin: Te olete jumalad“?
35 Kama aliwaita ‘miungu,’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
Ta nimetas neid inimesi jumalateks − inimesteks, kellele tuli Jumala sõna − ja Pühakirja ei või muuta.
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’
Miks te siis ütlete, et see, kelle Isa välja valis ja maailma läkitas, teotab Jumalat, sest ma ütlesin „Ma olen Jumala Poeg“?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini,
Kui ma ei tee seda, mida teeb mu Isa, siis ärge mind uskuge.
38 lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ndani yake.”
Aga kui ma seda teen, siis isegi kui te mind ei usu, peaksite uskuma tõendite pärast, mida ma olen teinud. Nii saate teada ja mõista, et Isa on minus ja mina Isas.“
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
Taaskord üritasid nad teda kinni võtta, kuid ta pääses nende käest.
40 Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
Ta läks tagasi üle Jordani jõe kohta, kus Johannes oli ristimist alustanud, ja jäi sinna.
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
Tema juurde tuli palju inimesi ja nad ütlesid: „Johannes ei teinud imetegusid, aga kõik, mida ta selle mehe kohta rääkis, on täide läinud.“
42 Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
Paljud, kes seal olid, hakkasid Jeesusesse uskuma.

< Yohana 10 >