< Yohana 10 >
1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
Amen, amen I say to you: He that entereth not by the door into the sheepfold, but climbeth up another way, the same is a thief and a robber.
2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
But he that entereth in by the door is the shepherd of the sheep.
3 Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
To him the porter openeth; and the sheep hear his voice: and he calleth his own sheep by name, and leadeth them out.
4 Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
And when he hath let out his own sheep, he goeth before them: and the sheep follow him, because they know his voice.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
But a stranger they follow not, but fly from him, because they know not the voice of strangers.
6 Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
This proverb Jesus spoke to them. But they understood not what he spoke to them.
7 Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
Jesus therefore said to them again: Amen, amen I say to you, I am the door of the sheep.
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
All others, as many as have come, are thieves and robbers: and the sheep heard them not.
9 Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
I am the door. By me, if any man enter in, he shall be saved: and he shall go in, and go out, and shall find pastures.
10 Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
The thief cometh not, but for to steal, and to kill, and to destroy. I am come that they may have life, and may have it more abundantly.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
I am the good shepherd. The good shepherd giveth his life for his sheep.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
But the hireling, and he that is not the shepherd, whose own the sheep are not, seeth the wolf coming, and leaveth the sheep, and flieth: and the wolf catcheth, and scattereth the sheep:
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
And the hireling flieth, because he is a hireling: and he hath no care for the sheep.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua.
I am the good shepherd; and I know mine, and mine know me.
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
As the Father knoweth me, and I know the Father: and I lay down my life for my sheep.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili, inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu, hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
And other sheep I have, that are not of this fold: them also I must bring, and they shall hear my voice, and there shall be one fold and one shepherd.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
Therefore doth the Father love me: because I lay down my life, that I may take it again.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
No man taketh it away from me: but I lay it down of myself, and I have power to lay it down: and I have power to take it up again. This commandment have I received of my Father.
19 Kwa maneno haya Wayahudi waligawanyika.
A dissension rose again among the Jews for these words.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
And many of them said: He hath a devil, and is mad: why hear you him?
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
Others said: These are not the words of one that hath a devil: Can a devil open the eyes of the blind?
22 Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
And it was the feast of the dedication at Jerusalem: and it was winter.
23 Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
And Jesus walked in the temple, in Solomon’s porch.
24 Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
The Jews therefore came round about him, and said to him: How long dost thou hold our souls in suspense? If thou be the Christ, tell us plainly.
25 Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
Jesus answered them: I speak to you, and you believe not: the works that I do in the name of my Father, they give testimony of me.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
But you do not believe, because you are not of my sheep.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
My sheep hear my voice: and I know them, and they follow me.
28 nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn , aiōnios )
And I give them life everlasting; and they shall not perish for ever, and no man shall pluck them out of my hand. (aiōn , aiōnios )
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
That which my Father hath given me, is greater than all: and no one can snatch them out of the hand of my Father.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
I and the Father are one.
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
The Jews then took up stones to stone him.
32 lakini Yesu akawaambia, “Nimewaonyesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni ipi katika hiyo mnataka kunipiga mawe?”
Jesus answered them: Many good works I have shewed you from my Father; for which of these works do you stone me?
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ingawa ni mwanadamu unajifanya kuwa Mungu.”
The Jews answered him: For a good work we stone thee not, but for blasphemy; and because that thou, being a man, maketh thyself God.
34 Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Sheria ya kwamba, ‘Nimesema kuwa, ninyi ni miungu?’
Jesus answered them: Is it not written in your law: I said you are gods?
35 Kama aliwaita ‘miungu,’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
If he called them gods, to whom to word of God was spoken, and the scripture cannot be broken;
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’
Do you say of him whom the Father hath sanctified and sent into the world: Thou blasphemest, because I said, I am the Son of God?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini,
If I do not the works of my Father, believe me not.
38 lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ndani yake.”
But if I do, though you will not believe me, believe the works: that you may know and believe that the Father is in me, and I in the Father.
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
They sought therefore to take him; and he escaped out of their hands.
40 Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
And he went again beyond the Jordan, into that place where John was baptizing first; and there he abode.
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
And many resorted to him, and they said: John indeed did no sign.
42 Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
But all things whatsoever John said of this man, were true. And many believed in him.