< Yohana 10 >
1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
“Truly, truly, I tell you, whoever does not enter the sheepfold by the gate, but climbs in some other way, is a thief and a robber.
2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
But the one who enters by the gate is the shepherd of the sheep.
3 Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
The gatekeeper opens the gate for him, and the sheep listen for his voice. He calls his own sheep by name and leads them out.
4 Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
When he has brought out all his own, he goes on ahead of them, and his sheep follow him because they know his voice.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
But they will never follow a stranger; in fact, they will flee from him because they do not recognize his voice.”
6 Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
Jesus spoke to them using this illustration, but they did not understand what He was telling them.
7 Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
So He said to them again, “Truly, truly, I tell you, I am the gate for the sheep.
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
All who came before Me were thieves and robbers, but the sheep did not listen to them.
9 Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
I am the gate. If anyone enters through Me, he will be saved. He will come in and go out and find pasture.
10 Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
The thief comes only to steal and kill and destroy. I have come that they may have life, and have it in all its fullness.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
I am the good shepherd. The good shepherd lays down His life for the sheep.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
The hired hand is not the shepherd, and the sheep are not his own. When he sees the wolf coming, he abandons the sheep and runs away. Then the wolf pounces on them and scatters the flock.
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
The man runs away because he is a hired servant and is unconcerned for the sheep.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua.
I am the good shepherd. I know My sheep and My sheep know Me,
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
just as the Father knows Me and I know the Father. And I lay down My life for the sheep.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili, inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu, hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
I have other sheep that are not of this fold. I must bring them in as well, and they will listen to My voice. Then there will be one flock and one shepherd.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
The reason the Father loves Me is that I lay down My life in order to take it up again.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
No one takes it from Me, but I lay it down of My own accord. I have authority to lay it down and authority to take it up again. This charge I have received from My Father.”
19 Kwa maneno haya Wayahudi waligawanyika.
Again there was division among the Jews because of Jesus’ message.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
Many of them said, “He is demon-possessed and insane. Why would you listen to Him?”
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
But others replied, “These are not the words of a man possessed by a demon. Can a demon open the eyes of the blind?”
22 Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
At that time the Feast of Dedication took place in Jerusalem. It was winter,
23 Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
and Jesus was walking in the temple courts in Solomon’s Colonnade.
24 Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
So the Jews gathered around Him and demanded, “How long will You keep us in suspense? If You are the Christ, tell us plainly.”
25 Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
“I already told you,” Jesus replied, “but you did not believe. The works I do in My Father’s name testify on My behalf.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
But because you are not My sheep, you refuse to believe.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
My sheep listen to My voice; I know them, and they follow Me.
28 nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn , aiōnios )
I give them eternal life, and they will never perish. No one can snatch them out of My hand. (aiōn , aiōnios )
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
My Father who has given them to Me is greater than all. No one can snatch them out of My Father’s hand.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
I and the Father are one.”
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
At this, the Jews again picked up stones to stone Him.
32 lakini Yesu akawaambia, “Nimewaonyesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni ipi katika hiyo mnataka kunipiga mawe?”
But Jesus responded, “I have shown you many good works from the Father. For which of these do you stone Me?”
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ingawa ni mwanadamu unajifanya kuwa Mungu.”
“We are not stoning You for any good work,” said the Jews, “but for blasphemy, because You, who are a man, declare Yourself to be God.”
34 Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Sheria ya kwamba, ‘Nimesema kuwa, ninyi ni miungu?’
Jesus replied, “Is it not written in your Law: ‘I have said you are gods’?
35 Kama aliwaita ‘miungu,’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
If he called them gods to whom the word of God came—and the Scripture cannot be broken—
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’
then what about the One whom the Father sanctified and sent into the world? How then can you accuse Me of blasphemy for stating that I am the Son of God?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini,
If I am not doing the works of My Father, then do not believe Me.
38 lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ndani yake.”
But if I am doing them, even though you do not believe Me, believe the works themselves, so that you may know and understand that the Father is in Me, and I am in the Father.”
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
At this, they tried again to seize Him, but He escaped their grasp.
40 Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
Then Jesus went back across the Jordan to the place where John had first been baptizing, and He stayed there.
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
Many came to Him and said, “Although John never performed a sign, everything he said about this man was true.”
42 Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
And many in that place believed in Jesus.