< Yohana 1 >

1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
V začetku je bila Beseda in Beseda je bila z Bogom in Beseda je bila Bog.
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
Ista je bila v začetku z Bogom.
3 Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
Vse stvari so bile narejene po njem in brez njega ni bilo narejeno nič, kar je bilo narejeno.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
V njem je bilo življenje in življenje je bilo svetloba ljudem.
5 Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
In svetloba sveti v temi, tema pa je ni doumela.
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
Bil je človek, poslan od Boga, katerega ime je bilo Janez.
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
Ta isti je prišel za pričo, da pričuje o Svetlobi, da bodo vsi ljudje po njem lahko verovali.
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
Ni bil on ta Svetloba, ampak je bil poslan, da pričuje o tej Svetlobi.
9 Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
To je bila resnična Svetloba, ki razsvetljuje vsakega človeka, ki prihaja na svet.
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
Bil je na svetu in svet je bil narejen po njem, svet pa ga ni spoznal.
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
Prišel je k svojim lastnim, njegovi lastni pa ga niso sprejeli.
12 Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
Toda tolikim, kot so ga sprejeli, njim je on dal moč, da postanejo Božji sinovi, torej njim, ki verujejo v njegovo ime,
13 Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
ki so bili rojeni, ne iz krvi niti ne iz volje mesa niti ne iz volje moža, temveč iz Boga.
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
In Beseda je bila narejena meso in prebivala med nami (in zagledali smo njegovo slavo, slavo kot od edinorojenega od Očeta) polno milosti in resnice.
15 Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
Janez je pričeval o njem in klical, rekoč: »Ta je bil tisti, o katerem sem govoril: ›Kdor prihaja za menoj, je obstajal pred menoj, kajti bil je prej kakor jaz.‹«
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
In iz njegove polnosti smo vsi prejeli in to milost za milostjo.
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
Kajti postava je bila dana po Mojzesu, toda milost in resnica sta prišli po Jezusu Kristusu.
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
Noben človek nikoli ni videl Boga. Edinorojeni Sin, ki je v Očetovem naročju, on ga je razodel.
19 Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
In to je Janezovo pričevanje, ko so Judje poslali iz Jeruzalema duhovnike in Lévijevce, da ga vprašajo: »Kdo si ti?«
20 Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
In priznal je in ni zanikal, temveč priznal: »Jaz nisem Kristus.«
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
In vprašali so ga: »Kaj torej? Ali si Elija?« In reče: »Nisem.« »Ali si ti ta prerok?« In odgovoril je: »Ne.«
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
Potem so mu rekli: »Kdo si? Da bomo lahko dali odgovor tem, ki so nas poslali. Kaj praviš sam o sebi?«
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
Rekel je: »Jaz sem glas nekoga, ki kliče v divjini: ›Naredite Gospodovo pot ravno, ‹ kakor je rekel prerok Izaija.«
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
Ti pa, ki so bili poslani, so bili izmed farizejev.
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
In vprašali so ga ter mu rekli: »Zakaj potem krščuješ, če ti nisi ta Kristus niti Elija niti ta prerok?«
26 Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
Janez jim je odgovoril, rekoč: »Jaz krščujem z vodo, toda tam, med vami, stoji nekdo, ki ga vi ne poznate.
27 Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
On je ta, ki prihaja za menoj, in je pred menoj, čigar čevljev jermena nisem vreden odvezati.«
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
Te stvari so se zgodile v Betaniji, onstran Jordana, kjer je Janez krščeval.
29 Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
Naslednji dan zagleda Janez k njemu prihajati Jezusa in reče: »Glejte, Jagnje Božje, ki odvzema greh sveta.
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
To je on, o katerem sem rekel: ›Za menoj prihaja mož, ki je obstajal pred menoj, kajti bil je pred menoj.‹
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
In nisem ga poznal, vendar sem zato prišel krščevat z vodo, da bi se on razodel Izraelu.«
32 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
In Janez je izjavil, rekoč: »Videl sem Duha spuščati se z neba, kakor golobico in je ostal na njem.
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
In nisem ga poznal, toda kdor me je poslal, da krščujem z vodo, isti mi je rekel: ›Na kogar boš videl spuščati se Duha in ostajati na njem, isti je ta, ki krščuje s Svetim Duhom.‹
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
In videl sem in izjavil, da je ta Božji Sin.«
35 Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
Naslednji dan je Janez ponovno stal in dva izmed njegovih učencev
36 Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
in ko je gledal na Jezusa, medtem ko je hodil, reče: »Glej, Jagnje Božje!«
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
Dva učenca pa sta ga slišala govoriti in šla za Jezusom.
38 Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
Potem se je Jezus obrnil in ju videl slediti ter jima reče: »Kaj iščeta?« Rekla sta mu: »Rabi (kar prevedeno pomeni Učitelj), kje prebivaš?«
39 Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
Reče jima: »Pridita in poglejta.« Prišla sta in videla, kje prebiva ter ta dan ostala z njim, kajti bilo je okrog desete ure.
40 Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
Eden izmed dveh, ki sta slišala Janeza govoriti in sta mu sledila, je bil Andrej, brat Simona Petra.
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
Ta je najprej našel svojega lastnega brata Simona in mu rekel: »Našli smo Mesija, « kar je prevedeno, Kristusa.
42 Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
In privedel ga je k Jezusu. In ko ga je Jezus pogledal, je rekel: »Ti si Simon, Jonov sin. Imenoval se boš Kefa, « kar je po razlagi: ›Kamen.‹
43 Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
Naslednji dan je Jezus nameraval oditi naprej v Galilejo in najde Filipa ter mu reče: »Sledi mi.«
44 Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
Torej Filip pa je bil iz Betsajde, Andrejevega in Petrovega mesta.
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Filip najde Natánaela in mu reče: »Našli smo tistega, o katerem so Mojzes in preroki pisali v postavi, Jezusa iz Nazareta, Jožefovega sina.«
46 Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
Natánael pa mu je rekel: »Ali lahko iz Nazareta pride kakršnakoli dobra stvar?« Filip mu reče: »Pridi in poglej.«
47 Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
Jezus je videl k njemu prihajati Natánaela in reče o njem: »Glejte, pravi Izraelec, v katerem ni zvijače!«
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
Natánael mu reče: »Od kod me poznaš?« Jezus je odgovoril in mu rekel: »Preden te je Filip poklical, sem te videl, ko si bil pod figovim drevesom.«
49 Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
Natánael je odgovoril in mu reče: »Rabi, ti si Božji Sin. Ti si Izraelov Kralj.«
50 Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
Jezus je odgovoril in mu rekel: »Ker sem ti rekel: ›Videl sem te pod figovim drevesom, ‹ veruješ? Videl boš večje stvari kakor te.«
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
In reče mu: »Resnično, resnično, povem vam: ›Odslej boste videli odprta nebesa in Božje angele, ki se vzpenjajo in spuščajo nad Sinom človekovim.‹«

< Yohana 1 >