< Yohana 1 >
1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
在世界之初,道即已存在。这是上帝之道,道即上帝。
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
在万物之初,这道便与上帝同在。
3 Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
万物皆为他所造,没有上帝就没有世上的一切。
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
他是生命之源,这生命就是人之光。
5 Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
光照亮黑暗,黑暗不能将光熄灭。
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
上帝派一位叫做约翰的人前来,
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
证明和解释光,让众人通过他相信上帝。
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
约翰不是光,而是要来此为那光作见证。
9 Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
这真正的光来到世界,普照世人。
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
他就是世界,世界乃通过他创造而成,但世界却并不知晓他是谁。
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
他来到自己的子民身边,但他们却不接受他。
12 Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
但接受他就是相信他的人,他会赋予他们成为上帝儿女的权利。
13 Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
他们并非以人间方式诞生的儿女,不是人类欲望的结果或父亲做出的决定,而是由上帝诞生。
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
道变身人类,生活在人类中间,我们可以看到他的荣光,这是天父唯一之子的荣光,满溢恩典和真理。
15 Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
约翰为他作见证,向民众高声呼喊:“他就是我之前所说的那个人:‘在我之后到来的人,远比我重要得多,因为他早在我之前就已存在。’”
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
他生性慷慨,我们接受他的慷慨,不断获得恩典之礼。
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
律法借由摩西颁布,恩典和真理却是通过耶稣基督而存在。
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
从未有人见过唯一的上帝,只有距离天父最近之人,才能向我们展示何为上帝。
19 Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
犹太人从耶路撒冷派牧师和利未人来到约翰这里,问他:“你是谁?”以下便是约翰做出的公开呈明。
20 Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
约翰明确而坦诚地说:“我不是基督。”没有一丝犹豫。
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
他们问:“那么你是谁?是以利亚吗?” 他说:“不,我不是。” “是那位先知吗?” 他回答:“不是。”
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
他们再问:“那么你是谁?我们需要回复派我们前来之人。你认为你自己是谁?”
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
他说:“我就是荒野中的呼喊之声:‘修直主的路!’”他引用了以赛亚先知所说的一句话。
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
这些由法利赛人派来的牧师和利未人
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
问约翰:“你既然不是基督、不是以利亚、也不是那位先知,那么你为什么施洗?”
26 Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
约翰回答:“我只是用水施洗,但你们中却有一个人,你们并不认识。
27 Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
他在我之后到来,我即使给他解鞋带都不配。”
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
约翰在约旦河施洗,这一切就发生在约旦河远处的伯大尼。
29 Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
第二天,约翰见耶稣向他走来,就说:“看,这是上帝的羔羊,他可以去除这世间的罪!
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
这就是我说的那个人‘有一个人,在我之后到来,远比我重要的多,因为他早在我之前就已存在。’
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
我本来不认识他。但为了让他可以显现给以色列人,我才来此用水施洗。”
32 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
约翰又给出关于耶稣的证明:“我曾看见圣灵如鸽子般从天上降落,停留在他的身上。
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
我本来不认识他,但派我前来用水施洗的那个人对我说:‘如果你看见圣灵降下并停留在谁身上,谁就能用圣灵进行施洗。’
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
我看到了所发生的一切,所以才能见证他就是上帝之子。”
35 Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
第二天,约翰和他的两个门徒站在那里。
36 Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
约翰看见耶稣经过,就说:“看,这就是上帝的羔羊!”
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
那两个门徒听见他这番话,就开始跟随耶稣。
38 Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
耶稣转过身来,看见他们跟在身后,就问:“你们在寻找什么?”他们说:“拉比(意为‘老师’),你住在哪里?”
39 Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
他说:“来看看吧。”于是他们就跟随他,看到他所住的地方。当时是下午四点,这一天剩下的时间,他们都和耶稣待在一起。
40 Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
在听从约翰跟随耶稣的那两个人中,有一个人是西门(即彼得)的弟弟安得烈。
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
他先找到自己的哥哥西门,告诉他:“我们遇见弥赛亚了!”(“弥赛亚”意为“基督。”)
42 Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
然后他就带着西门去见耶稣。耶稣直接看着西门说:“你是约翰的儿子西门,但现在你叫做矶法。”(即“彼得。”)
43 Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
第二天,耶稣决定去加利利。路上遇见了腓力,就对他说:“跟随我吧!”
44 Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
腓力是伯赛大人,是安得烈和彼得的同乡。
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
腓力找到拿但业,告诉他:“我们遇见了摩西在律法书上所写,众先知所记载的那个人,他就是约瑟的儿子,拿撒勒人耶稣。”
46 Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
拿但业说:“拿撒勒?那里能出什么好事?”腓力说:“来看看就知道了!”
47 Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
耶稣看见拿但业向他走过来,这样评价他:“看,这是一位真正的以色列人!没有任何污点和过错。”
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
拿但业问他:“你怎么知道我呢?”耶稣回答:“在腓力招呼你之前,我看到你站在无花果树下。”
49 Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
拿但业欢呼道:“拉比,你是上帝之子,你是以色列的王!”
50 Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
耶稣说:“你相信我,就是因为我说‘我看见你在无花果树下’这句话吗?你看到的会更多!”
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
然后耶稣说:“告诉你实话,你将看见天空开启,上帝的天使在人子处上上下下。”