< Joeli 3 >
1 “Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
Car voici, en ces jours-là, et dans ce temps où je ramènerai les captifs de Juda et de Jérusalem,
2 nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
Je rassemblerai toutes les nations et les ferai descendre dans la vallée de Josaphat; et là j'entrerai en jugement avec eux au sujet de mon peuple et de mon héritage, Israël, qu'ils ont dispersé parmi les nations, en se partageant mon pays.
3 Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
Ils ont jeté le sort sur mon peuple; ils ont donné le jeune garçon pour une prostituée, et ils ont vendu la jeune fille pour du vin, et ils ont bu.
4 “Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
Et vous aussi, Tyr et Sidon, et toutes les contrées des Philistins, que me voulez-vous? Voulez-vous vous venger de moi? Si vous voulez vous venger de moi, je vous rendrai promptement et soudain sur la tête votre salaire.
5 Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
Car vous avez pris mon argent et mon or, et vous avez emporté dans vos temples mes joyaux précieux.
6 Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
Vous avez vendu les enfants de Juda et les enfants de Jérusalem aux enfants de Javan, afin de les éloigner de leur territoire.
7 “Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
Voici, je les ferai revenir du lieu où vous les avez vendus, et je ferai retomber sur votre tête votre salaire.
8 Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
Je vendrai vos fils et vos filles aux enfants de Juda; ils les vendront aux Sabéens, à un peuple lointain; car l'Éternel a parlé.
9 Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
Publiez ceci parmi les nations; préparez la guerre; réveillez les hommes vaillants; que tous les gens de guerre s'approchent, et qu'ils montent!
10 Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
Forgez de vos hoyaux des épées, et de vos serpes, des lances; et que le faible dise: Je suis fort!
11 Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
Hâtez-vous et venez, vous toutes les nations d'alentour, et rassemblez-vous. Là, ô Éternel! fais descendre tes hommes vaillants!
12 “Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
Que les nations se réveillent, et qu'elles montent à la vallée de Josaphat; car là je siégerai pour juger toutes les nations d'alentour.
13 Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
Mettez la faucille, car la moisson est mûre. Venez, foulez, car le pressoir est plein; les cuves regorgent, car leur malice est grande.
14 Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
Des multitudes, des multitudes dans la vallée du jugement! Car le jour de l'Éternel est proche, dans la vallée du jugement.
15 Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
Le soleil et la lune s'obscurcissent, et les étoiles retirent leur éclat.
16 Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
L'Éternel rugit de Sion, et de Jérusalem il fait entendre sa voix; les cieux et la terre sont ébranlés; mais l'Éternel est pour son peuple une retraite, et une forteresse pour les enfants d'Israël.
17 “Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
Et vous saurez que je suis l'Éternel votre Dieu, qui habite en Sion, la montagne de ma sainteté; et Jérusalem sera sainte, et les étrangers n'y passeront plus.
18 “Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
En ce jour-là les montagnes ruisselleront de moût, et le lait coulera des collines; l'eau coulera dans tous les ruisseaux de Juda, et une source sortira de la maison de l'Éternel et arrosera la vallée de Sittim.
19 Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
L'Égypte deviendra une désolation; Édom sera réduit en un désert affreux, à cause de la violence faite aux enfants de Juda, dont ils ont répandu le sang innocent dans leur pays.
20 Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
Mais Juda sera habité éternellement, et Jérusalem d'âge en âge.
21 Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”
Et je nettoierai leur sang que je n'avais point encore nettoyé. Et l'Éternel habitera en Sion.