< Joeli 3 >
1 “Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
Car voici qu'en ce temps, et en ces jours-là, quand J'aurai fait revenir de la captivité Juda et Jérusalem,
2 nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
J'assemblerai toutes les nations et les conduirai dans la vallée de Josaphat; là Je plaiderai avec elles pour Mon peuple et pour Israël, Mon héritage: car elles l'ont dispersé parmi les Gentils, qui se sont partagé Ma terre.
3 Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
Et ils ont tiré Mon peuple au sort, et ils ont livré des enfants à la prostitution, et ils ont vendu des jeunes filles pour du vin, et ils ont bu.
4 “Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
Or, qu'y a-t-il entre vous et Moi, Tyr, Sidon, Galilée des Philistins? Est-ce que vous pourrez user de représailles avec Moi? Ou Me garderez-vous rancune en votre cœur? Je vous rétribuerai, Moi, vite et sévèrement, sur vos têtes:
5 Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
Parce que vous avez pris Mon argent et Mon or; parce que vous avez porté dans vos temples Mes ornements précieux;
6 Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
parce que vous avez vendu aux fils des Grecs les fils de Juda et les fils de Jérusalem, pour les chasser de leurs frontières.
7 “Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
Mais voilà que Je les ramènerai des contrées où vous les avez conduits, et Je vous rétribuerai sur vos têtes.
8 Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
Et Je donnerai vos fils et vos filles aux fils de Juda, pour qu'ils les vendent comme captifs chez une nation lointaine; ainsi a parlé le Seigneur.
9 Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
Publiez ces choses parmi les Gentils; sanctifiez la guerre; excitez les combattants, vous tous hommes exercés aux armes; rassemblez-vous, et partez.
10 Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
Forgez des glaives avec vos socs de charrue, et, avec vos faux, des javelines. Que le faible lui-même dise: Je suis fort.
11 Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
Venez tous ensemble et entrez, vous nations d'alentour; vous, fils d'Israël, réunissez-vous là: que l'homme pacifique devienne un guerrier.
12 “Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
Que toutes les nations se lèvent; qu'elles se rendent dans la vallée de Josaphat; c'est là que Je siège pour juger les nations d'alentour.
13 Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
Envoyez des faucilles, car le vendangeur est prêt; entrez et foulez aux pieds les grappes, car le pressoir est plein; laissez déborder les cuves, car leur méchanceté a comble la mesure.
14 Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
Les échos ont retenti dans la vallée du jugement; car le jour du Seigneur est proche dans la vallée du jugement.
15 Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
Le soleil et la terre seront enveloppés de ténèbres, et les étoiles retireront leur lumière.
16 Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
Le Seigneur jettera de grands cris du haut de Sion; Il fera entendre Sa voix du haut de Jérusalem; le ciel et la terre trembleront; mais le Seigneur épargnera Son peuple, et Il fortifiera les fils d'Israël.
17 “Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
Et vous connaîtrez que Je suis le Seigneur votre Dieu, qui réside en Sion, sur la montagne sainte; et Jérusalem sera sainte, et les étrangers n'y passeront plus.
18 “Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
Et il arrivera qu'en ce jour-là les montagnes ruisselleront de douceur, et les collines de lait; et l'eau coulera de toutes les sources de Juda, et une fontaine jaillira de la maison du Seigneur, et elle abreuvera le val de Sétim.
19 Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
L'Égypte sera mise à néant; l'Idumée sera un champ de désolation, à cause des iniquités de ses fils contre Juda, parce qu'ils ont versé le sang innocent sur leur terre.
20 Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
Et la Judée sera habitée dans tous les siècles, et Jérusalem dans les générations des générations.
21 Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”
Et Je rechercherai leur sang, et Je n'absoudrai point ceux qui l'ont versé, et le Seigneur aura Son tabernacle en Sion.