< Joeli 3 >

1 “Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
For lo! in tho daies, and in that tyme, whanne Y schal turne the caitifte of Juda and of Jerusalem,
2 nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
Y schal gadere alle folkis, and Y schal lede hem in to the valei of Josephat; and Y schal dispute there with hem on my puple, and myn eritage Israel, whiche thei scateriden among naciouns; and thei departiden my lond, and senten lot on my puple;
3 Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
and thei settiden a knaue child in the bordel hous, and seelden a damesel for wyn, that thei schulden drynke.
4 “Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
But what to me and to you, thou Tire, and Sidon, and ech ende of Palestyns? Whethir ye schulen yelde vengyng to me? and if ye vengen you ayens me, soone swiftli Y schal yelde while to you on youre heed.
5 Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
Ye token awey my siluer and gold, and ye brouyten my desirable thingis and faireste thingis in to youre templis of idols.
6 Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
And ye selden the sones of Juda, and the sones of Jerusalem to the sones of Grekis, that ye schulden make hem fer fro her coostis.
7 “Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
Lo! Y schal reise hem fro the place in which ye seelden hem; and Y schal turne youre yeldyng in to youre heed.
8 Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
And Y schal sille youre sones and youre douytris in the hondis of the sones of Juda, and thei schulen selle hem to Sabeis, a fer folc, for the Lord spak.
9 Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
Crye ye this thing among hethene men, halewe ye batel, reise ye stronge men; alle men werriours, neiy, and stie.
10 Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
Beete ye togydere youre plowis in to swerdis, and youre mattokkis in to speeris; a sijk man seie, that Y am strong.
11 Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
Alle folkis, breke ye out, and come fro cumpas, and be ye gaderid togidere; there the Lord schal make thi stronge men to die.
12 “Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
Folkis rise togidere, and stie in to the valei of Josofat; for Y schal sitte there, to deme alle folkis in cumpas.
13 Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
Sende ye sikelis, `ether sithis, for ripe corn wexide; come ye, and go ye doun, for the pressour is ful; pressouris ben plenteuouse, for the malice of hem is multiplied.
14 Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
Puplis, puplis in the valei of kittyng doun; for the dai of the Lord is nyy in the valei of kittyng doun.
15 Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
The sunne and the moone ben maad derk, and sterris withdrowen her schynyng.
16 Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
And the Lord schal rore fro Sion, and schal yyue his vois fro Jerusalem, and heuenes and erthe schulen be mouyd; and the Lord is the hope of his puple, and the strengthe of the sones of Israel.
17 “Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
And ye schulen wite, that Y am youre Lord God, dwellynge in Sion, in myn hooli hil; and Jerusalem schal be hooli, and aliens schulen no more passe bi it.
18 “Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
And it schal be, in that dai mounteyns schulen droppe swetnesse, and litle hillis schulen flowe with mylke, and watris schulen go bi alle the ryueris of Juda; and a welle schal go out of the hous of the Lord, and schal moiste the stronde of thornes.
19 Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
Egipt schal be in to desolacioun, and Idume in to desert of perdicioun; for that that thei diden wickidli ayens the sones of Juda, and schedden out innocent blood in her lond.
20 Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
And Judee schal be enhabited with outen ende, and Jerusalem in to generacioun and in to generacioun.
21 Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”
And Y schal clense the blood of hem, which Y hadde not clensid; and the Lord schal dwelle in Syon.

< Joeli 3 >