< Joeli 2 >
1 Pigeni tarumbeta katika Sayuni; pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu. Wote waishio katika nchi na watetemeke, kwa kuwa siku ya Bwana inakuja. Iko karibu,
Toca la trompeta en Sión, ¡y hacer sonar una alarma en mi montaña sagrada! Que tiemblen todos los habitantes de la tierra, porque llega el día de Yahvé, porque está muy cerca:
2 siku ya giza na huzuni, siku ya mawingu na utusitusi. Kama mapambazuko yasambaavyo toka upande huu wa milima hata upande mwingine jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja. Jambo kama hili halijakuwepo tangu zamani wala halitakuwepo tena kamwe kwa vizazi vijavyo.
Un día de oscuridad y penumbra, un día de nubes y espesa oscuridad. Como el amanecer que se extiende sobre las montañas, un pueblo grande y fuerte; nunca ha habido algo parecido, ni habrá más después de ellos, incluso a los años de muchas generaciones.
3 Mbele yao moto unateketeza, nyuma yao miali ya moto inawaka kwa nguvu. Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni, nyuma yao ni jangwa lisilofaa: hakuna kitu kinachowaepuka.
Un fuego devora ante ellos, y detrás de ellos, arde una llama. La tierra es como el jardín del Edén ante ellos, y detrás de ellos, un desierto desolado. Sí, y nadie ha escapado de ellos.
4 Wanaonekana kama farasi; wanakwenda mbio kama askari wapanda farasi.
Su aspecto es como el de los caballos, y corren como jinetes.
5 Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.
Como el ruido de los carros en las cimas de los montes, saltan, como el ruido de una llama de fuego que devora el rastrojo, como un pueblo fuerte puesto en orden de batalla.
6 Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu; kila uso unabadilika rangi.
Ante su presencia los pueblos se angustian. Todos los rostros se han vuelto pálidos.
7 Wanashambulia kama wapiganaji wa vita; wanapanda kuta kama askari. Wote wanatembea katika safu, hawapotoshi safu zao.
Corren como hombres poderosos. Escalan el muro como guerreros. Cada uno de ellos marcha en su línea, y no se desvían del camino.
8 Hakuna anayemsukuma mwenzake; kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja. Wanapita katika vizuizi bila kuharibu safu zao.
Uno no empuja a otro. Cada uno marcha por su propio camino. Rompieron las defensas y no rompan filas.
9 Wanaenda kasi kuingia mjini; wanakimbia ukutani. Wanaingia ndani ya nyumba; kwa kuingilia madirishani kama wevi.
Se precipitan sobre la ciudad. Corren en la pared. Suben a las casas. Entran por las ventanas como ladrones.
10 Mbele yao dunia inatikisika, anga linatetemeka, jua na mwezi vinatiwa giza, na nyota hazitoi mwanga wake tena.
La tierra tiembla ante ellos. Los cielos tiemblan. El sol y la luna se oscurecen, y las estrellas retiran su brillo.
11 Bwana anatoa mshindo wa ngurumo mbele ya jeshi lake; majeshi yake hayana idadi, ni wenye nguvu nyingi wale ambao hutii agizo lake. Siku ya Bwana ni kuu, ni ya kutisha. Ni nani anayeweza kuistahimili?
Yahvé hace tronar su voz ante su ejército, porque sus fuerzas son muy grandes; porque es fuerte quien obedece su mandato; porque el día de Yahvé es grande y muy imponente, ¿y quién puede soportarlo?
12 “Hata sasa,” asema Bwana, “nirudieni kwa mioyo yenu yote, kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”
“Sin embargo, ahora mismo — dice Yahvé — vuélvete a mí con todo tu corazón, y con ayuno, llanto y luto”.
13 Rarueni mioyo yenu na siyo mavazi yenu. Mrudieni Bwana, Mungu wenu, kwa maana yeye ndiye mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo, huona huruma, hujizuia kuleta maafa.
Rasga tu corazón y no tus vestiduras, y vuélvete a Yahvé, tu Dios; porque es clemente y misericordioso, lento para la ira, y abundante en bondad amorosa, y se abstiene de enviar la calamidad.
14 Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma na kuacha baraka nyuma yake: sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji kwa ajili ya Bwana Mungu wenu.
¿Quién sabe? Puede que se vuelva y ceda, y dejar una bendición detrás de él, una ofrenda de comida y una ofrenda de bebida a Yahvé, tu Dios.
15 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, tangazeni saumu takatifu, liiteni kusanyiko takatifu.
¡Toca la trompeta en Sión! Santificar un ayuno. Convocar una asamblea solemne.
16 Wakusanyeni watu, wekeni wakfu kusanyiko; waleteni pamoja wazee, wakusanyeni watoto, wale wanyonyao maziwa. Bwana arusi na atoke chumbani mwake na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.
Reúne al pueblo. Santificar la asamblea. Reúne a los ancianos. Reúne a los niños, y a los que amamantan de pecho. Que el novio salga de su habitación, y la novia fuera de su cámara.
17 Makuhani, ambao wanahudumu mbele za Bwana, na walie katikati ya ukumbi wa Hekalu na madhabahu. Waseme, “Wahurumie watu wako, Ee Bwana. Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa, neno la dhihaka kati ya mataifa. Kwa nini wasemezane miongoni mwao, ‘Yuko wapi Mungu wao?’”
Que los sacerdotes, los ministros de Yahvé, lloren entre el pórtico y el altar, y que digan: “Perdona a tu pueblo, Yahvé, y no des tu herencia a los reproches, que las naciones se enseñoreen de ellos. ¿Por qué han de decir entre los pueblos, ¿Dónde está su Dios?”
18 Kisha Bwana atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake na kuwa na huruma juu ya watu wake.
Entonces Yahvé se puso celoso por su tierra, y se apiadó de su pueblo.
19 Bwana atawajibu: “Ninawapelekea nafaka, mvinyo mpya na mafuta, vya kuwatosha ninyi hadi mridhike kabisa; kamwe sitawafanya tena kitu cha kudharauliwa na mataifa.
Yahvé respondió a su pueblo, “Mira, te enviaré grano, vino nuevo y aceite, y estarás satisfecho con ellos; y no volveré a hacer de ti un oprobio entre las naciones.
20 “Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi, nikilisukuma ndani ya jangwa, askari wa safu za mbele wakienda ndani ya bahari ya mashariki na wale wa safu za nyuma katika bahari ya magharibi. Uvundo wake utapaa juu; harufu yake itapanda juu.” Hakika ametenda mambo makubwa.
Pero yo alejaré de ti al ejército del norte, y lo conducirá a una tierra estéril y desolada, su frente en el mar del este, y su espalda en el mar occidental; y su hedor surgirá, y su mal olor se elevará”. Seguro que ha hecho grandes cosas.
21 Usiogope, ee nchi; furahi na kushangilia. Hakika Bwana ametenda mambo makubwa.
Tierra, no tengas miedo. Alegraos y regocijaos, porque Yahvé ha hecho grandes cosas.
22 Msiogope, enyi wanyama pori, kwa kuwa mbuga za malisho yenu zinarudia ubichi. Miti nayo inazaa matunda, mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.
No tengáis miedo, animales del campo; porque los pastos del desierto brotan, porque el árbol da sus frutos. La higuera y la vid dan su fuerza.
23 Furahini, enyi watu wa Sayuni, shangilieni katika Bwana Mungu wenu, kwa kuwa amewapa mvua za vuli kwa kipimo cha haki. Anawapelekea mvua nyingi, mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.
“Alegraos, pues, hijos de Sión, y alégrate en Yahvé, tu Dios; pues te da la lluvia temprana en justa medida, y hace que la lluvia caiga para ti, la lluvia temprana y la lluvia tardía, como antes.
24 Sakafu za kupuria zitajaa nafaka, mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.
Las eras estarán llenas de trigo, y las cubas rebosarán de vino nuevo y aceite.
25 “Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige: parare, madumadu na tunutu, jeshi langu kubwa ambalo nililituma katikati yenu.
Te devolveré los años que se ha comido la langosta, la gran langosta, el saltamontes y la oruga, mi gran ejército, que envié entre vosotros.
26 Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe, na mtalisifu jina la Bwana Mungu wenu, ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu; kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.
Tendrás mucho que comer y estarás satisfecho, y alabarán el nombre de Yahvé, su Dios, que ha tratado maravillosamente contigo; y mi pueblo nunca más será decepcionado.
27 Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu, na kwamba hakuna mwingine; kamwe watu wangu hawataaibika tena.
Sabrás que estoy en medio de Israel, y que yo soy Yahvé, tu Dios, y no hay otro; y mi pueblo nunca más será decepcionado.
28 “Hata itakuwa, baada ya hayo, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.
“Después sucederá que derramaré mi Espíritu sobre toda la carne; y tus hijos y tus hijas profetizarán. Tus viejos soñarán sueños. Sus jóvenes verán visiones.
29 Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu.
Y también sobre los siervos y las siervas en aquellos días, Derramaré mi Espíritu.
30 Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu na duniani: damu, moto na mawimbi ya moshi.
Mostraré maravillas en los cielos y en la tierra: sangre, fuego y columnas de humo.
31 Jua litageuzwa kuwa giza na mwezi kuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ya Bwana ile kuu na ya kutisha.
El sol se convertirá en oscuridad, y la luna en sangre, antes de que llegue el gran y terrible día de Yahvé.
32 Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa. Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu kutakuwepo wokovu, kama Bwana alivyosema, miongoni mwa walionusurika ambao Bwana awaita.
Sucederá que quien invoque el nombre de Yahvé se salvará; porque en el monte Sión y en Jerusalén habrá quienes escapen, como ha dicho Yahvé, y entre el remanente, los que Yahvé llama.