< Joeli 1 >

1 Neno la Bwana ambalo lilimjia Yoeli mwana wa Pethueli.
Šis ir Tā Kunga vārds, kas notika uz Joēli, Petuēļa dēlu.
2 Sikilizeni hili, enyi wazee; sikilizeni, ninyi nyote mnaoishi katika nchi. Je, jambo kama hili lilishawahi kutokea katika siku zenu au katika siku za babu zenu?
Klausiet šo vārdu, vecaji, un atgriežat ausis, visi zemes iedzīvotāji! Vai tāda lieta notikusi jūsu dienās vai jūsu tēvu dienās?
3 Waelezeni watoto wenu, na watoto wenu wawaambie watoto wao, na watoto wao kwa kizazi kitakachofuata.
Sludinājiet to saviem bērniem, un lai jūsu bērni to stāsta saviem bērniem, un atkal viņu bērni nākamam augumam.
4 Kilichosazwa na kundi la tunutu nzige wakubwa wamekula, kilichosazwa na nzige wakubwa parare wamekula, kilichosazwa na parare madumadu wamekula.
Ko kāpuri atlicina, to ēd siseņi, un ko siseņi atlicina, to ēd vaboles un ko vaboles atlicina, to ēd kukaiņi.
5 Amkeni, enyi walevi, mlie! Pigeni yowe enyi wanywaji wote wa mvinyo, pigeni yowe kwa sababu ya mvinyo mpya, kwa kuwa mmenyangʼanywa kutoka midomoni mwenu.
Uzmostaties, piedzērušie, un raudiet! Un kauciet, visi vīna plītnieki, par to jauno vīnu, jo tas ir atrauts no jūsu mutes.
6 Taifa limevamia nchi yangu, lenye nguvu tena lisilo na idadi; lina meno ya simba, magego ya simba jike.
Jo tauta ceļas pret manu zemi, varena un neskaitāma; viņas zobi ir lauvas zobi, un dzerokļi viņai ir kā vecam lauvam.
7 Limeharibu mizabibu yangu na kuangamiza mitini yangu. Limebambua magome yake na kuyatupilia mbali, likayaacha matawi yake yakiwa meupe.
Tā ir izpostījusi manu vīna koku un par žagariem darījusi manu vīģes koku; viņa to mizot ir nomizojusi un nometusi, viņa zari ir palikuši balti.
8 Omboleza kama bikira aliyevaa nguo ya gunia anayehuzunika kwa ajili ya mume wa ujana wake.
Vaidi kā jumprava, ar maisu apjozusies, sava jaunības brūtgāna dēļ.
9 Sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji zimekatiliwa mbali kutoka nyumba ya Bwana. Makuhani wanaomboleza, wale wanaohudumu mbele za Bwana.
Ēdamais upuris un dzeramais upuris ir atrauts no Tā Kunga nama; priesteri, Tā Kunga sulaiņi, bēdājās.
10 Mashamba yameharibiwa, ardhi imekauka; nafaka imeharibiwa, mvinyo mpya umekauka, mafuta yamekoma.
Tīrums ir postīts, zeme noskumusi, jo labība ir postīta, vīns sakaltis un eļļa iet bojā.
11 Kateni tamaa, enyi wakulima, lieni, enyi mlimao mizabibu; huzunikeni kwa ajili ya ngano na shayiri, kwa sababu mavuno ya shambani yameharibiwa.
Arāji paliek kaunā, vīna dārznieki kauc par kviešiem un miežiem, jo tīruma pļaušana ir pagalam.
12 Mzabibu umekauka na mtini umenyauka; mkomamanga, mtende na mtofaa, miti yote shambani, imekauka. Hakika furaha yote ya mwanadamu imeondoka.
Vīna koks ir sakaltis un vīģes koks iet bojā, granātābele un palmu koks un ābele, visi koki laukā ir nokaltuši, un līksmība ir nonīkusi pie cilvēku bērniem.
13 Vaeni nguo ya gunia, enyi makuhani, muomboleze; pigeni yowe, enyi mnaohudumu madhabahuni. Njooni, vaeni nguo ya gunia usiku kucha, enyi mnaohudumu mbele za Mungu wangu; kwa kuwa sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji zimezuiliwa kufika katika nyumba ya Mungu wenu.
Apjožaties un žēlojaties, priesteri, kauciet, altāra sulaiņi, ejat, paliekat maisos cauru nakti, mana Dieva sulaiņi, jo ēdamais upuris un dzeramais upuris ir atrauts no mana Dieva nama.
14 Tangazeni saumu takatifu; liiteni kusanyiko takatifu. Iteni wazee na wote waishio katika nchi waende katika nyumba ya Bwana Mungu wenu, wakamlilie Bwana.
Svētījat gavēni, izsauciet sapulces dienu, sapulcinājiet vecajus, visus zemes iedzīvotājus uz Tā Kunga, sava Dieva, namu un piesauciet To Kungu.
15 Ole kwa siku hiyo! Kwa kuwa siku ya Bwana iko karibu; itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
Ak vai, par to dienu! Jo Tā Kunga diena ir tuvu un nāks kā posts no tā Visuvarenā.
16 Je, chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu: furaha na shangwe kutoka nyumba ya Mungu wetu?
Vai barība priekš mūsu acīm nav atrauta, prieks un līksmība no mūsu Dieva nama?
17 Mbegu zinakauka chini ya mabonge ya udongo. Ghala zimeachwa katika uharibifu, ghala za nafaka zimebomolewa, kwa maana hakuna nafaka.
Graudi apakš zemes satrūdējuši, mantu nami ir tukši, šķūņi sagruvuši, jo labība nokaltusi.
18 Jinsi gani ngʼombe wanavyolia! Makundi ya mifugo yanahangaika kwa sababu hawana malisho; hata makundi ya kondoo yanateseka.
Ak, kā vaid lopi! Vēršu ganāmie pulki apstulbuši, jo tiem nav ganības, un avju pulki iet bojā.
19 Kwako, Ee Bwana, naita, kwa kuwa moto umeteketeza malisho ya mbugani na miali ya moto imeunguza miti yote shambani.
Tevi, ak Kungs, es piesaucu, jo uguns ir aprijis tuksneša ganības, un liesma ir iededzinājusi visus kokus laukā.
20 Hata wanyama wa porini wanakuonea shauku; vijito vya maji vimekauka, na moto umeteketeza malisho yote ya mbugani.
Pat zvēri laukā Tevi piesauc, jo ūdensupes izsīkušas, un uguns ir aprijis tuksneša ganības.

< Joeli 1 >