< Ayubu 1 >
1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
Ûs ülkesinde Eyüp adında bir adam yaşardı. Kusursuz, doğru bir adamdı. Tanrı'dan korkar, kötülükten kaçınırdı.
2 Alikuwa na wana saba na binti watatu,
Yedi oğlu, üç kızı vardı.
3 naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
Yedi bin koyuna, üç bin deveye, beş yüz çift öküze, beş yüz çift eşeğe ve pek çok köleye sahipti. Doğudaki insanların en zengini oydu.
4 Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
Oğulları sırayla evlerinde şölen verir, birlikte yiyip içmek için üç kızkardeşlerini de çağırırlardı.
5 Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
Bu şölen dönemi bitince Eyüp onları çağırtıp kutsardı. Sabah erkenden kalkar, “Çocuklarım günah işlemiş, içlerinden Tanrı'ya sövmüş olabilirler” diyerek her biri için yakmalık sunu sunardı. Eyüp hep böyle yapardı.
6 Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
Bir gün ilahi varlıklar RAB'bin huzuruna çıkmak için geldiklerinde, Şeytan da onlarla geldi.
7 Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
RAB Şeytan'a, “Nereden geliyorsun?” dedi. Şeytan, “Dünyada gezip dolaşmaktan” diye yanıtladı.
8 Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
RAB, “Kulum Eyüp'e bakıp da düşündün mü?” dedi, “Çünkü dünyada onun gibisi yoktur. Kusursuz, doğru bir adamdır. Tanrı'dan korkar, kötülükten kaçınır.”
9 Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
Şeytan, “Eyüp Tanrı'dan boşuna mı korkuyor?” diye yanıtladı.
10 Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
“Onu, ev halkını, sahip olduğu her şeyi sen çitle çevirip korumadın mı? Elleriyle yaptığı her şeyi bereketli kıldın. Sürüleri bütün ülkeye yayıldı.
11 Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
Ama elini uzatır da sahip olduğu her şeyi yok edersen, yüzüne karşı sövecektir.”
12 Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
RAB Şeytan'a, “Peki” dedi, “Sahip olduğu her şeyi senin eline bırakıyorum, yalnız kendisine dokunma.” Böylece Şeytan RAB'bin huzurundan ayrıldı.
13 Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
Bir gün Eyüp'ün oğullarıyla kızları ağabeylerinin evinde yemek yiyip şarap içerken
14 akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
bir ulak gelip Eyüp'e şöyle dedi: “Öküzler çift sürüyor, eşekler onların yanında otluyordu.
15 Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
Sabalılar baskın yaptı, hepsini alıp götürdü. Uşakları kılıçtan geçirdiler. Yalnız ben kaçıp kurtuldum sana durumu bildirmek için.”
16 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
O daha sözünü bitirmeden başka bir ulak gelip, “Tanrı ateş yağdırdı” dedi, “Koyunlarla uşakları yakıp küle çevirdi. Yalnızca ben kaçıp kurtuldum durumu sana bildirmek için.”
17 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
O daha sözünü bitirmeden başka bir ulak gelip, “Kildaniler üç bölük halinde develere saldırdı” dedi, “Hepsini alıp götürdüler, uşakları kılıçtan geçirdiler. Yalnızca ben kurtuldum durumu sana bildirmek için.”
18 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
O daha sözünü bitirmeden başka bir ulak gelip, “Oğullarınla kızların ağabeylerinin evinde yemek yiyip şarap içerken
19 ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
ansızın çölden şiddetli bir rüzgar esti” dedi, “Evin dört köşesine çarptı; ev gençlerin üzerine yıkıldı, hepsi öldü. Yalnız ben kurtuldum durumu sana bildirmek için.”
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
Bunun üzerine Eyüp kalktı, kaftanını yırtıp saçını sakalını kesti, yere kapanıp tapındı.
21 na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
Dedi ki, “Bu dünyaya çıplak geldim, çıplak gideceğim. RAB verdi, RAB aldı, RAB'bin adına övgüler olsun!”
22 Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.
Bütün bu olaylara karşın Eyüp günah işlemedi ve Tanrı'yı suçlamadı.