< Ayubu 1 >

1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
Oasr mwet se pangpang Job, su muta in acn Uz. El sie mwet su alu nu sin God, ac el arulana inse pwaye nu sel. El sie mwet na wo, ac el arulana karinganang tuh elan tia oru kutena ma koluk.
2 Alikuwa na wana saba na binti watatu,
Oasr wen itkosr ac acn tolu natul.
3 naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
Oasr pac itkosr tausin sheep, tolu tausin camel, cow tausin se, ac donkey lumfoko natul. Oayapa oasr mwet kulansap puspis lal, ac el kasrup liki mwet nukewa ke facl ma oan kutulap in acn Canaan.
4 Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
Kais sie wen itkosr natul Job inge ac muta orek kufwa, na tamulel uh kewa ac tuku nu kac, ac pacl nukewa elos ac suli pac tamtael tolu wialos in wi pac tuku nu kac.
5 Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
Ke lotu se tukun pacl in kufwa nukewa, Job el ac toangna tukakek ac orek kisa lun kais sie tulik inge in aknasnasyalosla. El oru ouinge mweyen el mu sahp sie selos tuh kaskas koluk lain God ke seasmak lal uh.
6 Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
Ke sun pacl se ma lipufan uh ac tuku nu ye mutun LEUM GOD, Satan el wi pac tuku.
7 Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
Na LEUM GOD El siyuk sel, “Kom muta ya tuku?” Na Satan el topuk ac fahk, “Nga forfor na, rarauni faclu.”
8 Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
Na LEUM GOD El fahk, “Ya kom liyal Job, mwet kulansap luk ah? Wangin sie mwet fin faclu wo ac inse pwaye nu sik oana el. El alu nu sik ac arulana taran elan tia orala kutena ma koluk.”
9 Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
Na Satan el fahk, “Ya Job el alu nu sum ke wangin?
10 Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
Kom nuna karinganul wi sou lal ac ma nukewa lal. Kom akinsewowoye ma nukewa el oru, ac kom sang cow na pus natul, ekoslana acn uh.
11 Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
Tusruktu kom fin eisla ma lal inge nukewa lukel, el ac ngetot nu sum ac selngawikomi!”
12 Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
Na LEUM GOD El fahk nu sel Satan, “Kwal, ma nukewa lal Job oan inpoum, tusruktu taranna kom in tia oru kutena ma nu ke manol Job.” Ouinge Satan el som.
13 Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
Sie len ah ke tulik natul Job elos tukeni ac orek kufwa in lohm sin wen se ma matu oemeet wialos ah,
14 akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
na mwet utuk kas se kasrusr tuku nu ke lohm sel Job ac fahk, “Kut tuh orekmakin ox uh in kihling acn ah, ac donkey ah muta inima se ma apkuran nu yen kut orekma we.
15 Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
Na mwet Sabea elos tuku orek lokoalok, ac pisrala nufon kosro inge. Elos uniya nufon mwet kulansap lom, ac nga mukena kaingla ngan tuh fahkot nu sum.”
16 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
Meet liki safla ma el fahk uh, sie pac mwet kulansap ah tuku ac fahk, “Sarom ah uniya sheep ac mwet karingin ah nufon. Nga mukena kaingla ngan tuh fahkot nu sum.”
17 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
Na meet liki safla sramsram lal ah, sie pac mwet kulansap ah tuku ac fahk, “U tolu sin mwet Chaldea elos tuku orek lokoalok nu sesr ac usla camel uh, ac uniya mwet kulansap lom nukewa sayuk. Nga mukena kaingla ngan tuh fahkot nu sum.”
18 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
El srakna sramsram, na sie pac mwet kulansap ah tuku ac fahk, “Tulik nutum ah orek kufwa in lohm sin wen matu se nutum ah,
19 ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
na polo eng na upa se tuhme yen mwesis ah me. Eng sac ikruiya lohm sac twe onelosla nufon. Nga mukena kaingla tuku ngan tuh fahkot nu sum.”
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
Na Job el tuyak ac seya nuknuk lal ah ke asor. El kalla nufon aunsifal ac putati oankiyuki nu infohk uh.
21 na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
Ac el fahk, “Nga isusla pisinpo, ac nga ac misa pisinpo. LEUM GOD El tuh ase, na pa inge El sifil eisla. Lela Inel in kaksakinyuk!”
22 Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.
Ma upa inge nukewa ne sikyak nu sel Job, a el tiana tafongla ac sis nu fin God koluk uh.

< Ayubu 1 >