< Ayubu 1 >

1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
Der levede engang i Landet Uz en mand ved Navn Job. Det var en from og retsindig Mand, der frygtede Gud og veg fra det onde.
2 Alikuwa na wana saba na binti watatu,
Syv Sønner og tre Døtre fødtes ham;
3 naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
og hans Ejendom udgjorde 7000 Stykker Småkvæg, 3000 Kameler, 500 Spand Okser, 500 Aseninder og såre mange Trælle, så han var mægtigere end alle Østens Sønner.
4 Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
Hans Sønner havde for Skik at holde Gæstebud på Omgang hos hverandre, og de indbød deres tre Søstre til at spise og drikke sammen med sig.
5 Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
Når så Gæstebudsdagene havde nået Omgangen rundt, sendte Job Bud og lod Sønnerne hellige sig, og tidligt om Morgenen ofrede han Brændofre, et for hver af dem. Thi Job sagde: "Måske har mine Sønner syndet og forbandet Gud i deres Hjerte." Således gjorde Job hver Gang.
6 Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
Nu hændte det en Dag, at Guds Sønner kom og trådte frem for HERREN, og iblandt dem kom også Satan.
7 Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
HERREN spurgte Satan: "Hvor kommer du fra?" Satan svarede HERREN: "Jeg har gennemvanket Jorden på Kryds og tværs."
8 Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
HERREN spurgte da Satan: " Har du lagt Mærke til min Tjener Job? Der findes ingen som han på Jorden, så from og retsindig en Mand, som frygter Gud og viger fra det onde."
9 Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
Men Satan svarede HERREN: "Mon det er for intet, Job frygter Gud?
10 Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
Har du ikke omgærdet ham og hans Hus og alt, hvad han ejer, på alle Kanter? Hans Hænders Idræt har du velsignet, og hans Hjorde breder sig i Landet.
11 Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
Men ræk engang din Hånd ud og rør ved alt, hvad han ejer! Sandelig, han vil forbande dig lige op i dit Ansigt!"
12 Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
Da sagde HERREN til Satan: "Se, alt hvad han ejer, er i din Hånd; kun mod ham selv må du ikke udrække din Hånd!" Så gik Satan bort fra HERRENs Åsyn.
13 Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
Da nu en Dag hans Sønner og Døtre spiste og drak i den ældste Broders Hus,
14 akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
kom et Sendebud til Job og sagde: "Okserne gik for Ploven, og Aseninderne græssede i Nærheden;
15 Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
så faldt Sabæerne over dem og tog dem; Karlene huggede de ned med Sværdet; jeg alene undslap for at melde dig det."
16 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
Medens han endnu talte, kom en anden og sagde: "Guds Ild faldt ned fra Himmelen og slog ned iblandt Småkvæget og Karlene og fortærede dem; jeg alene undslap for at melde dig det."
17 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
Medens han endnu talte, kom en tredje og sagde: "Kaldæerne kom i tre Flokke og kastede sig over Kamelerne og tog dem; Karlene huggede de ned med Sværdet; jeg alene undslap for at melde dig det."
18 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
Medens han endnu talte, kom en fjerde og sagde: "Dine Sønner og Døtre spiste og drak i deres ældste Broders Hus;
19 ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
og se, da for der et stærkt Vejr hen over Ørkenen, og det tog i Husets fire Hjørner, så det styrtede ned over de unge Mænd, og de omkom; jeg alene undslap for at melde dig det."
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
Da stod Job op, sønderrev sin Kappe, skar sit Hovedhår af og kastede sig til Jorden, tilbad
21 na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
og sagde: Nøgen kom jeg af Moders Skød, og nøgen vender jeg did tilbage. HERREN gav, og HERREN tog, HERRENs Navn være lovet!"
22 Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.
I alt dette syndede Job ikke og tillagde ikke Gud noget vrangt.

< Ayubu 1 >