< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi Mshuhi akajibu:
ויען בלדד השוחי ויאמר׃
2 “Hata lini wewe utasema mambo kama haya? Maneno yako ni kama upepo mkuu.
עד אן תמלל אלה ורוח כביר אמרי פיך׃
3 Je, Mungu hupotosha hukumu? Je, Mwenyezi hupotosha kile kilicho haki?
האל יעות משפט ואם שדי יעות צדק׃
4 Watoto wako walipomtenda dhambi, aliwapa adhabu ya dhambi yao.
אם בניך חטאו לו וישלחם ביד פשעם׃
5 Lakini ukimtafuta Mungu, nawe ukamsihi Mwenyezi,
אם אתה תשחר אל אל ואל שדי תתחנן׃
6 ikiwa wewe ni safi na mnyofu, hata sasa atainuka mwenyewe kwa niaba yako, na kukurudisha katika mahali pako pa haki.
אם זך וישר אתה כי עתה יעיר עליך ושלם נות צדקך׃
7 Ijapokuwa mwanzo wako ulikuwa mdogo, lakini mwisho wako utakuwa wa mafanikio.
והיה ראשיתך מצער ואחריתך ישגה מאד׃
8 “Ukaulize vizazi vilivyotangulia na uone baba zao walijifunza nini,
כי שאל נא לדר רישון וכונן לחקר אבותם׃
9 kwa kuwa sisi tumezaliwa jana tu na hatujui lolote, nazo siku zetu duniani ni kama kivuli tu.
כי תמול אנחנו ולא נדע כי צל ימינו עלי ארץ׃
10 Je, hawatakufundisha na kukueleza? Je, hawataleta maneno kutoka kwenye kufahamu kwao?
הלא הם יורוך יאמרו לך ומלבם יוצאו מלים׃
11 Je, mafunjo yaweza kumea mahali pasipo na matope? Matete yaweza kustawi bila maji?
היגאה גמא בלא בצה ישגה אחו בלי מים׃
12 Wakati bado yanaendelea kukua kabla ya kukatwa, hunyauka haraka kuliko majani mengine.
עדנו באבו לא יקטף ולפני כל חציר ייבש׃
13 Huu ndio mwisho wa watu wote wanaomsahau Mungu; vivyo hivyo matumaini ya wasiomjali Mungu huangamia.
כן ארחות כל שכחי אל ותקות חנף תאבד׃
14 Lile analolitumainia huvunjika upesi; lile analolitegemea ni utando wa buibui.
אשר יקוט כסלו ובית עכביש מבטחו׃
15 Huutegemea utando wake, lakini hausimami; huungʼangʼania, lakini haudumu.
ישען על ביתו ולא יעמד יחזיק בו ולא יקום׃
16 Yeye ni kama mti ulionyeshewa vizuri wakati wa jua, ukieneza machipukizi yake bustanini;
רטב הוא לפני שמש ועל גנתו ינקתו תצא׃
17 huifunganisha mizizi yake kwenye lundo la mawe, na kutafuta nafasi katikati ya mawe.
על גל שרשיו יסבכו בית אבנים יחזה׃
18 Unapongʼolewa kutoka mahali pake, ndipo mahali pale huukana na kusema, ‘Mimi kamwe sikukuona.’
אם יבלענו ממקומו וכחש בו לא ראיתיך׃
19 Hakika uhai wake hunyauka, na kutoka udongoni mimea mingine huota.
הן הוא משוש דרכו ומעפר אחר יצמחו׃
20 “Hakika Mungu hamkatai mtu asiye na hatia, wala kuitia nguvu mikono ya mtenda mabaya.
הן אל לא ימאס תם ולא יחזיק ביד מרעים׃
21 Bado atakijaza kinywa chako na kicheko, na midomo yako na kelele za shangwe.
עד ימלה שחוק פיך ושפתיך תרועה׃
22 Adui zako watavikwa aibu, nazo hema za waovu hazitakuwepo tena.”
שנאיך ילבשו בשת ואהל רשעים איננו׃

< Ayubu 8 >