< Ayubu 7 >
1 “Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani? Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
地上の人には、激しい労務があるではないか。またその日は雇人の日のようではないか。
2 Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni, au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
奴隷が夕暮を慕うように、雇人がその賃銀を望むように、
3 ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili, nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
わたしは、むなしい月を持たせられ、悩みの夜を与えられる。
4 Wakati nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’ Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
わたしは寝るときに言う、『いつ起きるだろうか』と。しかし夜は長く、暁までころびまわる。
5 Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu, ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
わたしの肉はうじと土くれとをまとい、わたしの皮は固まっては、またくずれる。
6 “Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
わたしの日は機のひよりも速く、望みをもたずに消え去る。
7 Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi; macho yangu kamwe hayataona tena raha.
記憶せよ、わたしの命は息にすぎないことを。わたしの目は再び幸を見ることがない。
8 Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena; utanitafuta, wala sitakuwepo.
わたしを見る者の目は、かさねてわたしを見ることがなく、あなたがわたしに目を向けられても、わたしはいない。
9 Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena. (Sheol )
雲が消えて、なくなるように、陰府に下る者は上がって来ることがない。 (Sheol )
10 Kamwe harudi tena nyumbani mwake; wala mahali pake hapatamjua tena.
彼は再びその家に帰らず、彼の所も、もはや彼を認めない。
11 “Kwa hiyo sitanyamaza; nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu, nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
それゆえ、わたしはわが口をおさえず、わたしの霊のもだえによって語り、わたしの魂の苦しさによって嘆く。
12 Je, mimi ni bahari, au mnyama mkubwa mno akaaye vilindini, hata uniweke chini ya ulinzi?
わたしは海であるのか、龍であるのか、あなたはわたしの上に見張りを置かれる。
13 Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji, nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
『わたしの床はわたしを慰め、わたしの寝床はわが嘆きを軽くする』とわたしが言うとき、
14 ndipo wanitisha kwa ndoto na kunitia hofu kwa maono,
あなたは夢をもってわたしを驚かし、幻をもってわたしを恐れさせられる。
15 hivyo ninachagua kujinyonga na kufa, kuliko huu mwili wangu.
それゆえ、わたしは息の止まることを願い、わが骨よりもむしろ死を選ぶ。
16 Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.
わたしは命をいとう。わたしは長く生きることを望まない。わたしに構わないでください。わたしの日は息にすぎないのだから。
17 “Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
人は何者なので、あなたはこれを大きなものとし、これにみ心をとめ、
18 kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
朝ごとに、これを尋ね、絶え間なく、これを試みられるのか。
19 Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
いつまで、あなたはわたしに目を離さず、つばをのむまも、わたしを捨てておかれないのか。
20 Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
人を監視される者よ、わたしが罪を犯したとて、あなたに何をなしえようか。なにゆえ、わたしをあなたの的とし、わたしをあなたの重荷とされるのか。
21 Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”
なにゆえ、わたしのとがをゆるさず、わたしの不義を除かれないのか。わたしはいま土の中に横たわる。あなたがわたしを尋ねられても、わたしはいないでしょう」。