< Ayubu 7 >

1 “Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani? Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
Non ha forse un duro lavoro l'uomo sulla terra e i suoi giorni non sono come quelli d'un mercenario?
2 Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni, au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
Come lo schiavo sospira l'ombra e come il mercenario aspetta il suo salario,
3 ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili, nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
così a me son toccati mesi d'illusione e notti di dolore mi sono state assegnate.
4 Wakati nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’ Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
Se mi corico dico: «Quando mi alzerò?». Si allungano le ombre e sono stanco di rigirarmi fino all'alba.
5 Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu, ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
Ricoperta di vermi e croste è la mia carne, raggrinzita è la mia pelle e si disfà.
6 “Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
I miei giorni sono stati più veloci d'una spola, sono finiti senza speranza.
7 Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi; macho yangu kamwe hayataona tena raha.
Ricordati che un soffio è la mia vita: il mio occhio non rivedrà più il bene.
8 Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena; utanitafuta, wala sitakuwepo.
Non mi scorgerà più l'occhio di chi mi vede: i tuoi occhi saranno su di me e io più non sarò.
9 Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena. (Sheol h7585)
Una nube svanisce e se ne va, così chi scende agl'inferi più non risale; (Sheol h7585)
10 Kamwe harudi tena nyumbani mwake; wala mahali pake hapatamjua tena.
non tornerà più nella sua casa, mai più lo rivedrà la sua dimora.
11 “Kwa hiyo sitanyamaza; nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu, nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
Ma io non terrò chiusa la mia bocca, parlerò nell'angoscia del mio spirito, mi lamenterò nell'amarezza del mio cuore!
12 Je, mimi ni bahari, au mnyama mkubwa mno akaaye vilindini, hata uniweke chini ya ulinzi?
Son io forse il mare oppure un mostro marino, perché tu mi metta accanto una guardia?
13 Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji, nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
Quando io dico: «Il mio giaciglio mi darà sollievo, il mio letto allevierà la mia sofferenza»,
14 ndipo wanitisha kwa ndoto na kunitia hofu kwa maono,
tu allora mi spaventi con sogni e con fantasmi tu mi atterrisci.
15 hivyo ninachagua kujinyonga na kufa, kuliko huu mwili wangu.
Preferirei essere soffocato, la morte piuttosto che questi miei dolori!
16 Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.
Io mi disfaccio, non vivrò più a lungo. Lasciami, perché un soffio sono i miei giorni.
17 “Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
Che è quest'uomo che tu nei fai tanto conto e a lui rivolgi la tua attenzione
18 kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
e lo scruti ogni mattina e ad ogni istante lo metti alla prova?
19 Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
Fino a quando da me non toglierai lo sguardo e non mi lascerai inghiottire la saliva?
20 Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
Se ho peccato, che cosa ti ho fatto, o custode dell'uomo? Perché m'hai preso a bersaglio e ti son diventato di peso?
21 Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”
Perché non cancelli il mio peccato e non dimentichi la mia iniquità? Ben presto giacerò nella polvere, mi cercherai, ma più non sarò!

< Ayubu 7 >