< Ayubu 7 >

1 “Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani? Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
הלא-צבא לאנוש על- (עלי-) ארץ וכימי שכיר ימיו
2 Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni, au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
כעבד ישאף-צל וכשכיר יקוה פעלו
3 ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili, nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
כן הנחלתי לי ירחי-שוא ולילות עמל מנו-לי
4 Wakati nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’ Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
אם-שכבתי-- ואמרתי מתי אקום ומדד-ערב ושבעתי נדדים עדי-נשף
5 Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu, ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
לבש בשרי רמה וגיש (וגוש) עפר עורי רגע וימאס
6 “Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
ימי קלו מני-ארג ויכלו באפס תקוה
7 Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi; macho yangu kamwe hayataona tena raha.
זכר כי-רוח חיי לא-תשוב עיני לראות טוב
8 Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena; utanitafuta, wala sitakuwepo.
לא-תשורני עין ראי עיניך בי ואינני
9 Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena. (Sheol h7585)
כלה ענן וילך כן יורד שאול לא יעלה (Sheol h7585)
10 Kamwe harudi tena nyumbani mwake; wala mahali pake hapatamjua tena.
לא-ישוב עוד לביתו ולא-יכירנו עוד מקמו
11 “Kwa hiyo sitanyamaza; nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu, nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
גם-אני לא אחשך-פי אדברה בצר רוחי אשיחה במר נפשי
12 Je, mimi ni bahari, au mnyama mkubwa mno akaaye vilindini, hata uniweke chini ya ulinzi?
הים-אני אם-תנין כי-תשים עלי משמר
13 Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji, nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
כי-אמרתי תנחמני ערשי ישא בשיחי משכבי
14 ndipo wanitisha kwa ndoto na kunitia hofu kwa maono,
וחתתני בחלמות ומחזינות תבעתני
15 hivyo ninachagua kujinyonga na kufa, kuliko huu mwili wangu.
ותבחר מחנק נפשי מות מעצמותי
16 Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.
מאסתי לא-לעלם אחיה חדל ממני כי-הבל ימי
17 “Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
מה-אנוש כי תגדלנו וכי-תשית אליו לבך
18 kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
ותפקדנו לבקרים לרגעים תבחננו
19 Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
כמה לא-תשעה ממני לא-תרפני עד-בלעי רקי
20 Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
חטאתי מה אפעל לך-- נצר האדם למה שמתני למפגע לך ואהיה עלי למשא
21 Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”
ומה לא-תשא פשעי-- ותעביר את-עוני כי-עתה לעפר אשכב ושחרתני ואינני

< Ayubu 7 >