< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Y Job respondió y dijo:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
¡Si solo pudiera medirse mi pena, y ponerla en la balanza contra mi problema!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Porque entonces su peso sería más que la arena de los mares, debido a esto mis palabras han sido cortadas.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Porque las flechas del Todopoderoso están dentro de mí, y su veneno bebe mi espíritu, su ejército de temores se pone en orden contra mí.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
¿El asno de los campos emite su voz cuando tiene pasto? ¿O el buey hace sonidos sobre su comida?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
¿Tomará un hombre comida que no tenga sabor sin sal? ¿O hay algún sabor en la clara del huevo?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Mi alma no desea tales cosas, son como enfermedades en mi comida.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
¡Si tan solo pudiera tener una respuesta a mi oración, y Dios me diera mi deseo!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
Si solo él se complaciera en terminar conmigo; ¡Y soltaría su mano para destruirme!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Por lo tanto, todavía tendría consuelo y gozaría con los dolores de la muerte, porque siempre he respetado las palabras del Dios Santo.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
¿Tengo fuerzas para seguir esperando o tengo algún fin para estar esperando?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
¿Es mi fortaleza la fuerza de las piedras, o es mi carne de bronce?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
No tengo ayuda en mí mismo, y la sabiduría se me ha ido por completo.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
El que tiene el corazón cerrado contra su amigo que sufre, ha renunciado al temor del Todopoderoso.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mis amigos han sido desleales como un arroyo, como arroyos en los valles que llegan a su fin.
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Que son oscuros por el hielo y la nieve que cae en ellos;
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Bajo el ardiente sol se secan, y no llegan a nada debido al calor.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Las caravanas de camellos se desvían de su camino; van al vacío y son destruidos.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Las caravanas de camellos de Tema los buscaron y de Saba, los esperaban.
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
Ellos vinieron, fueron avergonzados por su esperanza; y confundida su esperanza.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Así son ustedes ahora; Ven mi triste condición y tienen miedo.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
¿Dije, dame algo? o ¿Hacer un pago para mí de su riqueza?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
¿O me sacas del poder de mi enemigo? o ¿Dar dinero para que me rescaten del poder de los malvados?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Dame la enseñanza y estaré callado; Y hazme ver mi error.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
¡Qué agradables son las palabras rectas! ¿Pero qué prueba hay en tus argumentos?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Mis palabras pueden parecer malas, pero las palabras de quien no tiene esperanza son para el viento.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
En verdad, ustedes echarían suerte sobre un huérfano, y capaz de vender a su propio amigo.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Ahora pues, vuelvan sus ojos hacia mí, porque de verdad no diré lo que es falso en mi rostro.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Deja que tu mente sea cambiada, y no tengas una mala opinión de mí; Sí, cambia, porque mi justicia todavía está en mí.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
¿Hay mal en mi lengua? ¿No puede mi paladar discernir destrucción?

< Ayubu 6 >