< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Y RESPONDIÓ Job y dijo:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
¡Oh si pesasen al justo mi queja y mi tormento, y se alzasen igualmente en balanza!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Porque pesaría aquél más que la arena del mar: y por tanto mis palabras son cortadas.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Porque las saetas del Todopoderoso están en mí, cuyo veneno bebe mi espíritu; y terrores de Dios me combaten.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
¿Acaso gime el asno montés junto á la hierba? ¿muge el buey junto á su pasto?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
¿Comeráse lo desabrido sin sal? ¿ó habrá gusto en la clara del huevo?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Las cosas que mi alma no quería tocar, por los dolores son mi comida.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
¡Quién me diera que viniese mi petición, y que Dios [me] otorgase lo que espero;
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
Y que pluguiera á Dios quebrantarme; que soltara su mano, y me deshiciera!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Y sería aún mi consuelo, si me asaltase con dolor sin dar más tregua, que yo no he escondido las palabras del Santo.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
¿Cuál es mi fortaleza para esperar aún? ¿y cuál mi fin para dilatar mi vida?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
¿Es mi fortaleza la de las piedras? ¿ó mi carne, es de acero?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
¿No me ayudo cuanto puedo, y el poder me falta del todo?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
El atribulado es consolado de su compañero: mas hase abandonado el temor del Omnipotente.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mis hermanos han mentido cual arroyo: pasáronse como corrientes impetuosas,
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Que están escondidas por la helada, y encubiertas con nieve;
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Que al tiempo del calor son deshechas, y en calentándose, desaparecen de su lugar;
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Apártanse de la senda de su rumbo, van menguando y piérdense.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Miraron los caminantes de Temán, los caminantes de Saba esperaron en ellas:
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
[Mas] fueron avergonzados por su esperanza; porque vinieron hasta ellas, y halláronse confusos.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Ahora ciertamente como ellas sois vosotros: que habéis visto el tormento, y teméis.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
¿Os he dicho yo: Traedme, y pagad por mí de vuestra hacienda;
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Y libradme de la mano del opresor, y redimidme del poder de los violentos?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Enseñadme, y yo callaré: y hacedme entender en qué he errado.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
¡Cuán fuertes son las palabras de rectitud! Mas ¿qué reprende el que reprende de vosotros?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
¿Pensáis censurar palabras, y los discursos de un desesperado, que son como el viento?
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
También os arrojáis sobre el huérfano, y hacéis hoyo delante de vuestro amigo.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Ahora pues, si queréis, mirad en mí, y [ved] si miento delante de vosotros.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Tornad ahora, y no haya iniquidad; volved aún [á considerar] mi justicia en esto.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
¿Hay iniquidad en mi lengua? ¿no puede mi paladar discernir las cosas depravadas?

< Ayubu 6 >