< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Entonces Job respondió:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
“Si se pudiera pesar mi dolor y poner mis problemas en una balanza
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
serían más pesados que la arena del mar. Por eso hablé tan precipitadamente.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Porque las flechas del Todopoderoso están en mí; su veneno mina mi espíritu. Los terrores de Dios están alineados contra mí.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
¿No rebuznan los burros salvajes cuando se les acaba la hierba? ¿No gime el ganado cuando no tiene comida?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
¿Se puede comer sin sal algo que no tiene sabor? ¿Tiene algún sabor la clara del huevo?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
No puedo tocar ningún alimento, ¡la sola idea me hace sentir enfermo!
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
¡Oh, si pudiera tener lo que realmente quiero, que Dios me diera lo que más deseo!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
¡Que Dios estuviera dispuesto a aplastarme hasta la muerte, que me dejara morir!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Pero aún me consuela saber, haciéndome feliz a través del dolor interminable, que nunca he rechazado las palabras de Dios.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
“¿Por qué debo seguir esperando si no tengo fuerzas? ¿Por qué debo seguir adelante si no sé lo que me va a pasar?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
¿Acaso soy fuerte como una roca? ¿Acaso soy de bronce?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
¿Cómo puedo ayudarme a mí mismo ahora que cualquier posibilidad de éxito ha desaparecido?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
Quien no es amable con un amigo ha dejado de respetar al Todopoderoso.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mis hermanos han actuado con el mismo engaño que un arroyo del desierto, aguas caudalosas en el desierto que se desvanecen.
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
El arroyo se desborda cuando está lleno de hielo oscuro y nieve derretida,
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
pero con el calor se seca y desaparece, esfumándose de donde estaba.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Las caravanas de camellos se apartan para buscar agua, pero no la encuentran y mueren.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Las caravanas de Tema buscaron, los viajeros de Saba se confiaron,
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
pero sus esperanzas se desvanecieron: llegaron y no encontraron nada.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
“Ahora no ayudan en nada. Así de simple: ven mi problema y tienen miedo.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
¿Les he pedido algo? ¿Acaso les he pedido que sobornen a alguien a mi favor, usando su propio dinero?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
¿Les he pedido que me rescaten de un enemigo? ¿Les he pedido que me salven de mis opresores?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Explíquenme esto y me callaré. Muéstrenme en qué me equivoco.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Las palabras sinceras son dolorosas, ¿pero qué prueban sus argumentos?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
¿Van a discutir sobre lo que he dicho, cuando las palabras de alguien desesperado deberían dejar que el viento se las lleve?
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
¡Son capaces de jugar a los dados para ganarle un huérfano, así como son capaces de regatear con su amigo!
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
¡Mírenme a los ojos y digan si les miento en la cara!
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
¡No hablen así! ¡No sean injustos! Lo que digo es correcto.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
No estoy diciendo mentiras. ¿Acaso no sabría yo mismo si me equivoco?”

< Ayubu 6 >