< Ayubu 6 >
Då tok Job til ords og svara:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
«Um dei mitt mismod vega vilde og få ulukka mi på vegti,
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
det tyngjer meir enn havsens sand; difor var ordi mine ville.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
For Allvalds pilar sit i meg, mi ånd lyt suga deira gift; Guds rædslor reiser seg til åtak.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Skrik asnet vel i grøne eng? Og rautar uksen ved sitt for?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Kven et det smerne utan salt? Kven finn vel smak i eggjekvite?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Det byd meg mot å røra slikt, det er som min utskjemde mat.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Å, fekk eg uppfyllt bøni mi! Gav Gud meg det eg vonar på!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
Ja, vild’ han berre knusa meg, med hand si min livstråd slita!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Då hadde endå eg mi trøyst; trass pina skulde glad eg hoppa! - Den Heilage sitt ord eg held på.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Kva er mi kraft, at eg skuld’ vona? Mi framtid, at eg skulde tola?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Er krafti mi som steinen sterk? Er kanskje kroppen min av kopar?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Mi hjelp hev heilt forlate meg; all kvart stydjepunkt er frå meg teke.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
Ein rådlaus treng av venen kjærleik, um enn han ottast Allvald ei.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Som bekken brørne mine sveik, lik bekkjefar som turkar ut.
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Fyrst gruggast dei av bråna is, og snø som blandar seg uti,
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
men minkar so i sumarsoli, og kverv til slutt burt i sumarhiten.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Vegfarande vik av til deim, men kjem til øydemark og døyr.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Kjøpmenn frå Tema skoda dit, flokkar frå Saba vonar trygt;
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
men svikne vert dei i si von; dei narra vert når dei kjem fram.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
So hev de vorte reint til inkjes, de rædsla såg, og rædde vart!
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Hev eg då bede dykk um noko? Bad eg dykk løysa meg med gods?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
og frelsa meg frå fiendvald og kjøpa meg frå røvarar?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Gjev meg eit svar, so skal eg tegja; seg meg kva eg hev synda med!
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Eit rettvis ord er lækjebot; men last frå dykk er inkje verdt.
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Du lastar meg for ordi mine; men vonlaus mann so mangt kann segja.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
De kastar lut um farlaust barn, og handel driv um dykkar ven.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Vilde de berre sjå på meg! Trur de eg lyg dykk upp i augo?
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Vend um, lat ikkje urett skje! Vend um, enn hev eg rett i dette.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Finst det vel fals på tunga mi? Kann ei min gom ulukka smaka?