< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Et Job reprit et dit:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Ah! qu'on pèse, qu'on pèse mon tourment! et qu'on mette mon malheur dans la balance aussi!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
car sur le sable des mers il l'emporte en grandeur: de là mes paroles outrées!
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Car je porte sur moi les flèches du Tout-puissant, de leur poison mon cœur est abreuvé; les terreurs de Dieu m'ont cerné.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
L'onagre brait-il auprès de la verdure? Le taureau mugit-il auprès de son fourrage?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Mange-t-on ce qui est insipide, sans sel? Le blanc de l'œuf a-t-il une saveur?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Mon âme refuse d'y toucher, et c'est comme une pourriture qui infecte mon pain.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
O, si mon vœu pouvait s'accomplir, et si Dieu remplissait mon souhait!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
S'il plaisait à Dieu de m'écraser, d'étendre sa main, et de me retrancher!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Ainsi j'aurais encore une consolation, et une joie dans les maux qu'il ne m'épargne pas, car je n'ai point renié la parole du Dieu Saint.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Qu'est-ce que ma force pour attendre? et qu'est-ce que ma fin, pour patienter?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Ma force est-elle la force de la pierre? mon corps est-il d'airain?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Par moi-même ne suis-je pas sans ressources, et le secours n'est-il pas refoulé loin de moi?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
A l'affligé son ami doit de l'affection, sinon il dépouille la crainte du Tout-puissant.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mes frères sont perfides comme le torrent, comme les eaux des ravins, qui tarissent,
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
que troublent les glaces, où s'enfonce la neige,
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
qui, au temps de leur baisse, se dissipent, et, quand vient la chaleur, leur lit se trouve à sec.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Les caravanes s'écartent de leur route, s'avancent dans le désert, et périssent;
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
là portent leurs regards les caravanes de Théma, là les voyageurs de Séba placent leur espérance;
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
ils ont honte d'avoir eu confiance, ils y arrivent, et sont confus.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
De même vous n'êtes rien, vous voyez la terreur, et tremblez.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Est-ce que j'ai dit: Donnez-moi! et avec vos biens, gagnez-moi la faveur!
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
et tirez-moi de la main de l'ennemi, et de la main des furieux rachetez-moi?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Instruisez-moi! je veux me taire, et faites-moi sentir en quoi j'ai failli!
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Quelle force dans le langage de la vérité! mais que démontrent vos remontrances?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Est-ce des discours que vous pensez à reprendre? mais on livre au vent les propos du désespoir.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Oui, sur l'orphelin vous jetez le filet, et vous creusez la fosse devant votre ami.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Mais ici, veuillez me regarder! et vos yeux vous diront si je suis un menteur.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Revenez donc! qu'il n'y ait pas injustice! revenez! j'ai encore raison sur ce point.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
L'injustice est-elle sur ma langue, et mon palais ne distingue-t-il pas ce qui est mauvais?

< Ayubu 6 >