< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Mais Job répondit, et dit:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Plût à Dieu que mon indignation fût bien pesée, et qu'on mît ensemble dans une balance ma calamité!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Car elle serait plus pesante que le sable de la mer; c'est pourquoi mes paroles sont englouties.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Parce que les flèches du Tout-puissant sont au dedans de moi; mon esprit en suce le venin; les frayeurs de Dieu se dressent en bataille contre moi.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
L'âne sauvage braira-t-il après l'herbe, et le bœuf mugira-t-il après son fourrage?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Mangera-t-on sans sel ce qui est fade? trouvera-t-on de la saveur dans le blanc d'un œuf?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Mais pour moi, les choses que je n'aurais pas seulement voulu toucher, sont des saletés qu'il faut que je mange.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Plût à Dieu que ce que je demande m'arrivât, et que Dieu me donnât ce que j'attends;
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
Et que Dieu voulût m'écraser, et [qu'il voulût] lâcher sa main pour m'achever!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Mais j'ai encore cette consolation, quoique la douleur me consume, et qu'elle ne m'épargne point, que je n'ai point tû les paroles du Saint.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Quelle est ma force, que je puisse soutenir [de si grands maux]? et quelle [en est] la fin, que je puisse prolonger ma vie?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Ma force est-elle une force de pierre, et ma chair est-elle d'acier?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Ne suis-je pas destitué de secours, et tout appui n'est-il pas éloigné de moi?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
A celui qui se fond [sous l'ardeur des maux, est due] la compassion de son ami; mais il a abandonné la crainte du Tout-puissant.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mes frères m'ont manqué comme un torrent, comme le cours impétueux des torrents qui passent;
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Lesquels on ne voit point à cause de la glace, et sur lesquels s'entasse la neige;
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Lesquels, au temps que la chaleur donne dessus, défaillent; quand ils sentent la chaleur, ils disparaissent de leur lieu;
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Lesquels serpentant çà et là par les chemins, se réduisent à rien, et se perdent.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Les troupes des voyageurs de Téma y pensaient, ceux qui vont en Séba s'y attendaient;
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
[Mais] ils sont honteux d'y avoir espéré; ils y sont allés, et ils en ont rougi.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Certes, vous m'êtes devenus inutiles; vous avez vu ma calamité étonnante, et vous en avez eu horreur.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Est-ce que je vous ai dit: Apportez-moi et me faites des présents de votre bien?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Et délivrez-moi de la main de l'ennemi, et me rachetez de la main des terribles?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Enseignez-moi, et je me tairai; et faites-moi entendre en quoi j'ai erré.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Ô combien sont fortes les paroles de vérité! mais votre censure, à quoi tend-elle?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Pensez-vous qu'il ne faille avoir que des paroles pour censurer; et que les discours de celui qui est hors d'espérance, ne soient que du vent?
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Vous vous jetez même sur un orphelin, et vous percez votre intime ami.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Mais maintenant je vous prie regardez-moi bien, si je mens en votre présence!
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Revenez, je vous prie, [et] qu'il n'y ait point d'injustice [en vous]; oui, revenez encore; car je ne suis point coupable en cela.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Y a-t-il de l'iniquité en ma langue? et mon palais ne sait-il pas discerner mes calamités?

< Ayubu 6 >