< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Alors Job répondit,
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
« Oh! si mon angoisse était pesée, et que toutes mes calamités soient mises dans la balance!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Car maintenant, il serait plus lourd que le sable des mers, c'est pourquoi mes paroles ont été irréfléchies.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Car les flèches du Tout-Puissant sont en moi. Mon esprit boit leur poison. Les terreurs de Dieu se sont dressées contre moi.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
L'âne sauvage braille-t-il quand il a de l'herbe? Ou le bœuf se penche-t-il sur son fourrage?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Peut-on manger sans sel ce qui n'a pas de saveur? Ou y a-t-il un goût dans le blanc d'un œuf?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Mon âme refuse de les toucher. Ils sont comme de la nourriture répugnante pour moi.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
« Oh, que je puisse avoir ma demande, que Dieu m'accorde la chose que je désire,
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
même qu'il plairait à Dieu de m'écraser; qu'il lâche sa main, et me coupe!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Qu'elle soit encore ma consolation, oui, laissez-moi exulter dans la douleur qui n'épargne pas, que je n'ai pas renié les paroles du Saint.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Quelle est ma force, pour que j'attende? Quelle est ma fin, pour que je sois patient?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Ma force est-elle la force des pierres? Ou ma chair est-elle de bronze?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
N'est-ce pas que je n'ai pas de secours en moi, que la sagesse est éloignée de moi?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
« A celui qui est prêt à s'évanouir, il faut que son ami fasse preuve de bonté; même à celui qui abandonne la crainte du Tout-Puissant.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mes frères ont agi de façon trompeuse comme un ruisseau, comme le canal des ruisseaux qui passent;
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
qui sont noirs à cause de la glace, dans laquelle la neige se cache.
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Pendant la saison sèche, ils disparaissent. Quand il fait chaud, ils sont consommés hors de leur place.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Les caravanes qui voyagent à côté d'eux se détournent. Ils montent dans le désert, et périssent.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Les caravanes de Tema regardaient. Les compagnies de Saba les attendaient.
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
Ils ont été affligés parce qu'ils étaient confiants. Ils sont arrivés là, et ont été confondus.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Car maintenant vous n'êtes rien. Vous voyez une terreur, et vous avez peur.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Ai-je jamais dit: « Donne-moi »? ou « Offrez-moi un cadeau de votre substance »?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
ou « Délivre-moi de la main de l'adversaire »? ou: « Délivre-moi de la main de l'oppresseur »?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
« Apprends-moi, et je me tairai. Fais-moi comprendre mon erreur.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Quelle force ont les paroles de la droiture! Mais votre réprobation, que réprouve-t-elle?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Avez-vous l'intention de réprouver les mots, puisque les discours de celui qui est désespéré sont comme du vent?
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Oui, vous tireriez même au sort pour l'orphelin, et faire de votre ami une marchandise.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Maintenant, regardez-moi avec plaisir, car je ne te mentirai pas en face.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Veuillez retourner. Qu'il n'y ait pas d'injustice. Oui, revenez encore. Ma cause est juste.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Y a-t-il de l'injustice sur ma langue? Mon goût ne peut-il pas discerner des choses malicieuses?

< Ayubu 6 >