< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Forsothe Joob answeride, and seide,
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Y wolde, that my synnes, bi whiche Y `desseruede ire, and the wretchidnesse which Y suffre, weren peisid in a balaunce.
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
As the grauel of the see, this wretchidnesse schulde appere greuousere; wherfor and my wordis ben ful of sorewe.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
For the arowis of the Lord ben in me, the indignacioun of whiche drynkith vp my spirit; and the dredis of the Lord fiyten ayens me.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Whether a feeld asse schal rore, whanne he hath gras? Ethir whether an oxe schal lowe, whanne he stondith byfor a `ful cratche?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Ether whethir a thing vnsauery may be etun, which is not maad sauery bi salt? Ether whether ony man may taaste a thing, which tastid bryngith deeth?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
For whi to an hungri soule, yhe, bittir thingis semen to be swete; tho thingis whiche my soule nolde touche bifore, ben now my meetis for angwisch.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Who yyueth, that myn axyng come; and that God yyue to me that, that Y abide?
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
And he that bigan, al to-breke me; releesse he his hond, and kitte me doun?
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
And `this be coumfort to me, that he turmente me with sorewe, and spare not, and that Y ayenseie not the wordis of the hooli.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
For whi, what is my strengthe, that Y suffre? ethir which is myn ende, that Y do pacientli?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Nethir my strengthe is the strengthe of stoonus, nether my fleisch is of bras.
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Lo! noon help is to me in me; also my meyneal frendis `yeden awey fro me.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
He that takith awei merci fro his frend, forsakith the drede of the Lord.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
My britheren passiden me, as a stronde doith, that passith ruschyngli in grete valeis.
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Snow schal come on hem, that dreden frost.
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
In the tyme wherynne thei ben scaterid, thei schulen perische; and as thei ben hoote, thei schulen be vnknyt fro her place.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
The pathis of her steppis ben wlappid; thei schulen go in veyn, and schulen perische.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Biholde ye the pathis of Theman, and the weies of Saba; and abide ye a litil.
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
Thei ben schent, for Y hopide; and thei camen `til to me, and thei ben hilid with schame.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Now ye ben comun, and now ye seen my wounde, and dreden.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Whether Y seide, Brynge ye to me, and yiue ye of youre catel to me? ethir,
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Delyuere ye me fro the hond of enemy, and rauysche ye me fro the hond of stronge men?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Teche ye me, and Y schal be stille; and if in hap Y vnknew ony thing, teche ye me.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Whi han ye depraued the wordis of trewthe? sithen noon is of you, that may repreue me.
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Ye maken redi spechis oneli for to blame, and ye bryngen forth wordis in to wynde.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Ye fallen in on a fadirles child, and enforsen to peruerte youre frend.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Netheles fille ye that, that ye han bigunne; yyue ye the eere, and se ye, whether Y lie.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Y biseche, answere ye with out strijf, and speke ye, and deme ye that, that is iust.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
And ye schulen not fynde wickidnesse in my tunge, nethir foli schal sowne in my chekis.

< Ayubu 6 >