< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Then Job answered and said:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
O that my grief were weighed thoroughly! That my calamities were put together in the balance!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Surely they would be heavier than the sand of the sea; On this account were my words rash.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
For the arrows of the Almighty have pierced me; Their poison drinketh up my spirit; The terrors of God set themselves in array against me.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Doth the wild ass bray in the midst of grass? Or loweth the ox over his fodder?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Can that which is unsavory be eaten without salt? Is there any taste in the white of an egg?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
That which my soul abhorreth to touch Hath become my loathsome food.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
O that I might have my request, And that God would grant me that which I long for!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
That it would please God to destroy me; That he would let loose his hand, and make an end of me!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Yet it should still be my consolation, Yea, in unsparing anguish I would exult, That I have not denied the commands of the Holy One.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
What is my strength, that I should hope? And what mine end, that I should be patient?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Is my strength the strength of stones? Or is my flesh brass?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Alas, there is no help within me! Deliverance is driven from me!
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
To the afflicted, kindness should be shown by a friend; Else he casteth off the fear of the Almighty.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
But my brethren are faithless like a brook; Like streams of the valley that pass away;
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Which are turbid by reason of the ice, And the snow, which hideth itself in them.
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
As soon as they flow forth, they vanish; When the heat cometh, they are dried up from their place.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
The caravans turn aside to them on their way; They go up into the desert, and perish.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
The caravans of Tema look for them; The companies of Sheba expect to see them;
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
They are ashamed that they have relied on them; They come to their place, and are confounded.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
So ye also are nothing; Ye see a terror, and shrink back.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Have I said, Bring me gifts? Or, Give a present for me out of your substance?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Or, Deliver me from the enemy's hand? Or, Rescue me from the hand of the violent?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Convince me, and I will hold my peace; Cause me to understand wherein I have erred.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
How powerful are the words of truth! But what do your reproaches prove?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Do ye mean to censure words? The words of a man in despair are but wind.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Truly ye spread a net for the fatherless; Ye dig a pit for your friend.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Look now upon me, I pray you; For to your very face can I speak falsehood?
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Return, I pray, and let there be no unfairness; Yea, return; —still is my cause righteous.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Is there iniquity on my tongue? Cannot my taste discern what is sinful?

< Ayubu 6 >