< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
And Job answered and said,
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Oh that my grief were thoroughly weighed, and all my calamity laid in the balances!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For now it would be heavier than the sand of the seas; therefore my words are vehement.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
For the arrows of the Almighty are within me, their poison drinketh up my spirit: the terrors of God are arrayed against me.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Doth the wild ass bray by the grass? loweth an ox over his fodder?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Shall that which is insipid be eaten without salt? Is there any taste in the white of an egg?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
What my soul refuseth to touch, that is as my loathsome food.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Oh that I might have my request, and that God would grant my desire!
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
And that it would please God to crush me, that he would let loose his hand and cut me off!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
Then should I yet have comfort; and in the pain which spareth not I would rejoice that I have not denied the words of the Holy One.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
What is my strength, that I should hope? and what is mine end, that I should have patience?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Is my strength the strength of stones? is my flesh of brass?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Is it not that there is no help in me, and soundness is driven away from me?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
For him that is fainting kindness [is meet] from his friend; or he forsaketh the fear of the Almighty.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
My brethren have dealt deceitfully as a stream, as the channel of streams which pass away,
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Which are turbid by reason of the ice, in which the snow hideth itself:
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
At the time they diminish, they are dried up; when heat affecteth them, they vanish from their place:
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
They wind about in the paths of their course, they go off into the waste and perish.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
The caravans of Tema looked, the companies of Sheba counted on them:
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
They are ashamed at their hope; they come thither, and are confounded.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
So now ye are nothing; ye see a terrible object and are afraid.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Did I say, Bring unto me, and make me a present from your substance?
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
Or, rescue me from the hand of the oppressor, and redeem me from the hand of the violent?
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Teach me, and I will hold my tongue; and cause me to understand wherein I have erred.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
How forcible are right words! but what doth your upbraiding reprove?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Do ye imagine to reprove words? The speeches of one that is desperate are indeed for the wind.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Yea, ye overwhelm the fatherless, and dig [a pit] for your friend.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Now therefore if ye will, look upon me; and it shall be to your face if I lie.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Return, I pray you, let there be no wrong; yea, return again, my righteousness shall be in it.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Is there wrong in my tongue? cannot my taste discern mischievous things?

< Ayubu 6 >