< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
But Job, responding, said:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
I wish that my sins, for which I deserve wrath, and the calamity that I endure, were weighed out on a balance.
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Compared to the sand of the sea, they would appear heavier, and so my words are full of sorrow.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
For the arrows of the Lord are in me, my spirit drinks of their indignation, and the terrors of the Lord are soldiers against me.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Will the wild ass bray when he has grass? Or will the ox bellow when he stands before a full manger?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Or can one eat bland food, which is not seasoned with salt? Or can anyone taste that which, if tasted, causes death?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
The things that my soul was unwilling to touch before, now, because of anguish, are my foods.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Who will grant that my petition may arrive and that God may bestow on me what I expect,
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
and that he who, at first, had crushed me, will let loose his hand and cut me down?
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
And may this be my consolation, that in afflicting me with sorrow, although he might not be lenient with me, I still do not contradict the words of the Holy One.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
For what is my strength, that I may continue? Or what is my goal, so that I may act patiently?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
My strength is not the strength of stones, nor is my flesh made of bronze.
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Behold, there is no help for me in myself, and my loved ones also have withdrawn from me.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
He who takes away mercy from his friend, abandons the fear of the Lord.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
My brethren have disregarded me, like a torrent that passes swiftly through the steep valleys.
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
Those who fear frost, snow will rush over them.
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
At that time, when they are scattered, they will perish, and when it becomes hot, they will be freed from their place.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
The paths of their steps are entangled; they will walk in vain and will perish.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Consider the paths of Thema, the ways of Saba, and wait a little while.
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
They have been thrown into confusion, just as I had hoped; they have even come to me and are overwhelmed with shame.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Now you have arrived, and merely by seeing my affliction, you are afraid.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Did I say: “Bring to me and give to me from your necessities?”
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
or, “Free me from the hand of the enemy and rescue me from the hand of the strong?”
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Teach me, and I will be silent, and if by chance I have been ignorant of anything, instruct me.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Why have you diminished the words of truth, when there is none of you who is able to offer proof against me?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
You prepare speeches as so much noise, and you offer words into the wind.
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
You encroach upon the orphan, and you strive to undermine your friend.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Such is true, so finish what you have begun. Listen closely, and see if I lie.
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Respond, I beg you, without contention, and, speaking what is just, pass judgment.
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
And you will not find iniquity on my tongue, nor will foolishness resound in my throat.

< Ayubu 6 >