< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Saa tog Job til Orde og svarede:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Gid man vejed min Harme og vejed min Ulykke mod den!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Thi tungere er den end Havets Sand, derfor talte jeg over mig!
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Thi i mig sidder den Almægtiges Pile, min Aand inddrikker deres Gift; Rædsler fra Gud forvirrer mig.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Skriger et Vildæsel midt i Græsset, brøler en Okse ved sit Foder?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Spiser man ferskt uden Salt, smager mon Æggehvide godt?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
Min Sjæl vil ej røre derved, de Ting er som Lugt af en Løve.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
Ak, blev mit Ønske dog opfyldt, Gud give mig det, som jeg haaber;
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
vilde Gud dog knuse mig, række Haanden ud og skære mig fra,
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
saa vilde det være min Trøst — jeg hopped af Glæde trods skaanselsløs Kval at jeg ikke har nægtet den Helliges Ord.
11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
Hvad er min Kraft, at jeg skal holde ud, min Udgang, at jeg skal være taalmodig?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
Er da min Kraft som Stenens, er da mit Legeme Kobber?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
Ak, for mig er der ingen Hjælp, hver Udvej lukker sig for mig.
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
Den, der nægter sin Næste Godhed, han bryder med den Almægtiges Frygt.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
Mine Brødre sveg mig som en Bæk, som Strømme, hvis Vand svandt bort,
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
de, der var grumset af os, og som Sneen gemte sig i,
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
men som svandt ved Solens Glød, tørredes sporløst ud i Hede;
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Karavaner bøjer af fra Vejen, drager op i Ørkenen og gaar til Grunde;
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Temas Karavaner spejder, Sabas Rejsetog haaber paa dem,
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
men de beskæmmes i deres Tillid, de kommer derhen og skuffes!
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
Ja, slige Strømme er I mig nu, Rædselen saa I og grebes af Skræk!
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
Har jeg mon sagt: »Giv mig Gaver, løs mig med eders Velstand,
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
red mig af Fjendens Haand, køb mig fri fra Voldsmænds Haand!«
24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
Lær mig, saa vil jeg tie, vis mig, hvor jeg har fejlet!
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
Redelig Tale, se, den gør Indtryk; men eders Revselse, hvad er den værd?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Er det jer Hensigt at revse Ord? Den fortvivledes Ord er dog Mundsvejr!
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
Selv om en faderløs kasted I Lod og købslog om eders Ven.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
Men vilde I nu dog se paa mig! Mon jeg lyver jer op i Ansigtet?
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
Vend jer hid, lad der ikke ske Uret, vend jer, thi end har jeg Ret!
30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Er der Uret paa min Tunge, eller skelner min Gane ej, hvad der er ondt?

< Ayubu 6 >