< Ayubu 5 >
1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Grita ahora por ayuda; ¿Hay alguien que te dé una respuesta? ¿Y a cuál de los santos harás tu oración?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Porque la ira es la causa de la muerte para los necios, y el que no tiene sabiduría llega a su fin a través de su envidia.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
He visto a los tontos echar raíces, pero de repente maldije su morada.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Ahora sus hijos no tienen un lugar seguro, y son destruidos en la puerta de la ciudad, y no hay nadie quien los libere.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Su cosecha es tomada por el hambriento, y aun de los espinos saca su grano, y el ladrón anhela sus riquezas.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Porque el mal no sale del polvo, ni los problemas salen de la tierra;
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Pero los problemas son causa del hombre desde el nacimiento, así como las chispas salen volando del fuego.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Pero en cuanto a mí, haría mi oración a Dios, y pondría mi causa delante de él.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Quien hace grandes cosas fuera de nuestro conocimiento, y maravillas innumerables:
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Que da lluvia sobre la tierra, y envía agua a los campos.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Levantando a los que están bajos, y poniendo a los tristes en un lugar seguro;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Que hace que los planes de los sabios vayan mal, de modo que no puedan cumplir sus propósitos.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Él atrapa a los astutos en sus planes secretos, y los propósitos de los malvados fracasan.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Durante el día se oscurece para ellos, y al mediodía andan a tientas como si fuera de noche.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Pero él guarda al pobre de la espada de su boca, y a los pobres del poderoso.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Entonces el pobre tiene esperanza, y la boca del malvado es detenida.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
En verdad, ese hombre es feliz, cuando lo reprende Dios: así que no dejes que tu corazón esté cerrado a la enseñanza del Dios Todopoderoso.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Porque después de su castigo él da consuelo, y después de herir, sus manos sanan.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Él te mantendrá a salvo de seis problemas, y en siete ningún mal se te acercará.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
Cuando haya necesidad de comida, él te guardará de la muerte, y en la guerra del poder de la espada.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Él te mantendrá a salvo de la lengua malvada; y no tendrás miedo de la destrucción cuando llegue.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Harás burla de la destrucción y del hambre, y no temerás a las bestias de la tierra.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Porque estarás de aliado con las piedras de la tierra, y las bestias del campo estarán en paz contigo.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Y estarás seguro de que tu tienda está en paz, y después de revisar tu propiedad verás que nada se ha perdido.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Estarás seguro de que tu simiente será numerosa y tu descendencia como las plantas de la tierra.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Llegarás a tu vejez con vigor, como él montón de trigo que se recoge a su tiempo.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Mira, lo hemos examinado con cuidado, y es así; óyelo; compruébalo por ti mismo.