< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
AHORA pues da voces, si habrá quien te responda; ¿y á cuál de los santos te volverás?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Es cierto que al necio la ira lo mata, y al codicioso consume la envidia.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
Yo he visto al necio que echaba raíces, y en la misma hora maldije su habitación.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Sus hijos estarán lejos de la salud, y en la puerta serán quebrantados, y no habrá quien los libre.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Su mies comerán los hambrientos, y sacaránla de entre las espinas, y los sedientos beberán su hacienda.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Porque la iniquidad no sale del polvo, ni la molestia brota de la tierra.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Empero como las centellas se levantan para volar por [el aire], así el hombre nace para la aflicción.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Ciertamente yo buscaría á Dios, y depositaría en él mis negocios:
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
El cual hace cosas grandes é inescrutables, y maravillas que no tienen cuento:
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Que da la lluvia sobre la haz de la tierra, y envía las aguas por los campos:
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Que pone los humildes en altura, y los enlutados son levantados á salud:
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Que frustra los pensamientos de los astutos, para que sus manos no hagan nada:
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Que prende á los sabios en la astucia de ellos, y el consejo de los perversos es entontecido;
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
De día se topan con tinieblas, y en mitad del día andan á tientas como de noche:
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Y libra de la espada al pobre, de la boca de los impíos, y de la mano violenta;
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Pues es esperanza al menesteroso, y la iniquidad cerrará su boca.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
He aquí, bienaventurado es el hombre á quien Dios castiga: por tanto no menosprecies la corrección del Todopoderoso.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Porque él es el que hace la llaga, y él [la] vendará: él hiere, y sus manos curan.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
En seis tribulaciones te librará, y en la séptima no te tocará el mal.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
En el hambre te redimirá de la muerte, y en la guerra de las manos de la espada.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Del azote de la lengua serás encubierto; ni temerás de la destrucción cuando viniere.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
De la destrucción y del hambre te reirás, y no temerás de las bestias del campo:
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Pues aun con las piedras del campo tendrás tu concierto, y las bestias del campo te serán pacíficas.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Y sabrás que hay paz en tu tienda; y visitarás tu morada, y no pecarás.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Asimismo echarás de ver que tu simiente es mucha, y tu prole como la hierba de la tierra.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Y vendrás en la vejez á la sepultura, como el montón de trigo que se coge á su tiempo.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
He aquí lo que hemos inquirido, lo cual es así: óyelo, y juzga tú para contigo.

< Ayubu 5 >