< Ayubu 5 >
1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
¡Clama ahora! ¿Habrá quién te responda? ¿A cuál de los santos acudirás?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Porque la ira mata al necio, y la envidia mata al simple.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
Vi al necio que echaba raíces, y al instante maldije su vivienda.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Sus hijos están lejos de toda seguridad. Son aplastados en la puerta y no habrá quién los defienda.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Su cosecha la devoran los hambrientos y aun la sacan de entre los espinos. Los sedientos sorben su hacienda.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Porque la aflicción no sale del polvo, ni el sufrimiento brota de la tierra,
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
sino el hombre nace para la aflicción, como las chispas salen hacia arriba.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Ciertamente yo buscaría a ʼElohim y encomendaría a Él mi causa,
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Quien hace cosas grandes e inescrutables, maravillas incontables.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Él da la lluvia a la tierra y envía el agua sobre la superficie de los campos.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Él exalta a los humildes y levanta a los enlutados a la seguridad.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Frustra los pensamientos de los astutos para que nada hagan sus manos y
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
atrapa a los sabios en su astucia. Frustra los designios del perverso.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Tropiezan de día con la oscuridad y a mediodía andan a tientas como de noche.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Así libra al pobre de la espada, de la boca de los poderosos y de su mano.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
El necesitado conserva la esperanza. La perversidad cierra su boca.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Dichoso el hombre a quien ʼElohim disciplina. No menosprecies la corrección de ʼEL-Shadday,
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
porque Él hace la herida, pero también la venda. Hiere, pero sus manos sanan.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Te librará de seis tribulaciones, y aun en la séptima no te tocará el mal.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
Durante la hambruna te librará de la muerte, y del poder de la espada en la guerra.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Estarás escondido del azote de la lengua, y no temerás cuando venga la destrucción.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Te reirás de la destrucción y de la hambruna y no temerás a las fieras del campo,
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
pues aun con las piedras del campo harás pacto, y las bestias del campo tendrán paz contigo.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Sabrás que hay paz en tu tienda. Nada te faltará cuando revises tu morada.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Verás también que tu descendencia es numerosa y tu prole como la hierba de la tierra.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Irás a la tumba en la vejez, como la gavilla de trigo que se recoge a su tiempo.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Mira que esto lo investigamos, es así. Óyelo, y conócelo por ti mismo.