< Ayubu 5 >
1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Призови же, аще кто тя услышит, или аще кого от святых Ангел узриши.
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Безумнаго бо убивает гнев, заблуждшаго же умерщвляет рвение.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
Аз же видех безумных укореняющихся, но абие поядено бысть их жилище.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Далече да будут сынове их от спасения, и да сотрутся при дверех хуждших, и не будет изимаяй.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Иже бо они собраша, праведницы поядят, сами же от зол не изяти будут: изможденна буди крепость их.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Не имать бо от земли изыти труд, ни от гор прозябнути болезнь:
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
но человек раждается на труд, птенцы же суповы высоко парят.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Обаче же аз помолюся Богови, Господа же всех Владыку призову,
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Творящаго велия и неизследимая, славная же и изрядная, имже несть числа:
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
дающаго дождь на землю, посылающаго воду на поднебесную:
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
возносящаго смиренныя на высоту и погибшыя воздвизающаго во спасение:
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
расточающаго советы лукавых, да не сотворят руце их истины.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Уловляяй премудрых в мудрости их, совет же коварных разори.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Во дни обымет их тма, в полудне же да осяжут якоже в нощи,
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
и да погибнут на брани: немощный же да изыдет из руки сильнаго.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Буди же немощному надежда, неправеднаго же уста да заградятся.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Блажен же человек, егоже обличи Бог, наказания же Вседержителева не отвращайся:
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Той бо болети творит и паки возставляет: порази, и руце Его изцелят:
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
шестижды от бед измет тя, в седмем же не коснеттися зло:
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
во гладе избавит тя от смерти, на брани же из руки железа изрешит тя:
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
от бича языка скрыет тя, и не убоишися от зол находящих:
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
неправедным и беззаконным посмеешися, от дивиих же зверей не убоишися,
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
зане с камением дивиим завет твой: зверие бо дивии примирятся тебе.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Потом уразумееши, яко в мире будет дом твой, жилище же храмины твоея не имать согрешити:
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
уразумееши же, яко много семя твое, и чада твоя будут яко весь злак селный:
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
внидеши же во гроб якоже пшеница созрелая во время пожатая, или якоже стог гумна во время свезенный.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Се, сия сице изследихом: сия суть, яже слышахом: ты же разумей себе, аще что сотворил еси.