< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Zawołajże tedy, jeźli kto jest, coćby odpowiedział? a do któregoż się z świętych obrócisz?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Zaiste głupiego zabija gniew, a prostaka umarza zawiść.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
Jam widział głupiego, iż się rozkorzenił; alem wnet źle tuszył mieszkaniu jego.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Oddaleni będą synowie jego od zbawienia, i starci będą w bramie, a nie będzie, ktoby ich wyrwał.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Żniwo jego głodny pożre, i z samego ciernia wybierze je; a połknie chciwy bogactwa takowych.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Albowiem nie z prochu wychodzi utrapienie, ani z ziemi wyrasta kłopot.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Ale człowiek na kłopot się rodzi jako iskry z węgla latają w górę.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Zaiste jabym szukał Boga, Bogubym przełożył sprawę swoję;
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Który czyni rzeczy wielkie i niewybadane, dziwne, którym liczby niemasz;
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Który daje deszcz na ziemię, i spuszcza wody na pola;
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Który sadza pokornych wysoko, a smutnych wywyższa ku zbawieniu;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Który w niwecz obraca myśli chytrych, tak, iż ręce ich nie sprawią nic skutecznego;
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Który chwyta mądrych w chytrości ich, a radę przewrotnych prędko niszczy.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
We dnie taczają się jako w ciemnościach, a jako w nocy macają w południe.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Który zachowuje ubogiego od miecza, od ust ich, i od ręki gwałtownika.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Mać uciśniony nadzieje; ale nieprawość stuli usta swe.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Oto błogosławiony człowiek, którego Bóg karze; przetoż karaniem Wszechmocnego nie pogardzaj,
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Bo on zrania i zawiązuje; uderza, a ręce jego uzdrawiają.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Z sześciu ucisków wyrwie cię, a w siódmym nie tknie się ciebie złe.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
W głodzie wybawi cię od śmierci, a na wojnie z rąk miecza.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Przed biczem języka ukryty będziesz, a nie ulękniesz się w spustoszeniu, gdy przyjdzie.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
W spustoszeniu i w głodzie śmiać się będziesz, a zwierząt ziemskich bać się nie będziesz.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Bo z kamieniem polnym będzie przymierze twoje, a okrutny zwierz polny spokojnym ci się stawi.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
I poznasz, że jest spokojny przybytek twój, i nawiedzisz mieszkanie twoje, a nie zgrzeszysz.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Doznasz też, iż rozmnożone będzie nasienie twoje, a potomstwo twoje będzie jako ziele ziemi.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Wnijdziesz w sędziwości do grobu, jako znoszone bywa zboże w stóg czasu swego.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Otośmy tego doszli, że tak jest: słuchajże tego, a uważaj to sam u siebie.

< Ayubu 5 >