< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Crie maintenant! Y aura-t-il quelqu'un qui te réponde? Et vers lequel des saints te tourneras-tu?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
La colère tue l'insensé, et le dépit fait mourir celui qui est destitué de sens;
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
J'ai vu l'insensé étendant ses racines, mais soudain j'ai maudit sa demeure.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Ses fils sont loin de tout secours, ils sont écrasés à la porte, et personne ne les délivre;
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
L'affamé dévore sa moisson; il la lui prend à travers les épines de sa haie; l'homme altéré convoite ses biens.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Car la souffrance ne sort pas de la poussière, et la peine ne germe pas du sol,
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
De sorte que l'homme soit né pour la peine, comme l'étincelle pour voler en haut.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Mais moi, j'aurais recours à Dieu, et j'adresserais ma parole à Dieu,
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Qui fait de grandes choses qu'on ne peut sonder, de merveilleuses choses qu'on ne peut compter;
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Qui répand la pluie sur la face de la terre, et qui envoie les eaux sur la face des champs;
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Qui met en haut ceux qui sont abaissés, et ceux qui sont en deuil au faîte du bonheur;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Qui dissipe les projets des hommes rusés, et leurs mains ne viennent à bout de rien;
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Qui prend les sages dans leurs propres ruses, et le dessein des pervers est renversé.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
De jour, ils rencontrent les ténèbres, et, comme dans la nuit, ils tâtonnent en plein midi;
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Et il délivre le pauvre de l'épée de leur bouche, et de la main des puissants.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Et il y a une espérance pour les malheureux, et la méchanceté a la bouche fermée.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Voici, heureux l'homme que Dieu châtie! Ne méprise donc pas la correction du Tout-Puissant.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Car c'est lui qui fait la plaie et la bande; il blesse et ses mains guérissent.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Dans six détresses, il te délivrera; et dans sept, le mal ne te touchera point.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
En temps de famine, il te garantira de la mort, et en temps de guerre, du tranchant de l'épée.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Tu seras à couvert du fléau de la langue, et tu n'auras point peur de la désolation, quand elle arrivera.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Tu riras de la dévastation et de la famine, et tu n'auras pas peur des bêtes de la terre;
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Car tu auras un pacte avec les pierres des champs, et les bêtes des champs seront en paix avec toi.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Et tu verras la prospérité dans ta tente: tu visiteras tes pâturages,
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Et rien ne t'y manquera; et tu verras ta postérité croissante, et tes descendants pareils à l'herbe de la terre.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Tu entreras mûr dans le tombeau, comme une gerbe qu'on emporte en son temps.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Voilà, nous avons examiné la chose; elle est ainsi, écoute cela, et fais-en ton profit.

< Ayubu 5 >