< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Crie maintenant! Qui te répondra? Auquel des saints t’adresseras-tu?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
L’insensé périt dans sa colère, Le fou meurt dans ses emportements.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
J’ai vu l’insensé prendre racine; Puis soudain j’ai maudit sa demeure.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Plus de prospérité pour ses fils; Ils sont foulés à la porte, et personne qui les délivre!
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Sa moisson est dévorée par des affamés, Qui viennent l’enlever jusque dans les épines, Et ses biens sont engloutis par des hommes altérés.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Le malheur ne sort pas de la poussière, Et la souffrance ne germe pas du sol;
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
L’homme naît pour souffrir, Comme l’étincelle pour voler.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Pour moi, j’aurais recours à Dieu, Et c’est à Dieu que j’exposerais ma cause.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Il fait des choses grandes et insondables, Des merveilles sans nombre;
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Il répand la pluie sur la terre, Et envoie l’eau sur les campagnes;
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Il relève les humbles, Et délivre les affligés;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Il anéantit les projets des hommes rusés, Et leurs mains ne peuvent les accomplir;
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Il prend les sages dans leur propre ruse, Et les desseins des hommes artificieux sont renversés:
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Ils rencontrent les ténèbres au milieu du jour, Ils tâtonnent en plein midi comme dans la nuit.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Ainsi Dieu protège le faible contre leurs menaces, Et le sauve de la main des puissants;
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Et l’espérance soutient le malheureux, Mais l’iniquité ferme la bouche.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Heureux l’homme que Dieu châtie! Ne méprise pas la correction du Tout-Puissant.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Il fait la plaie, et il la bande; Il blesse, et sa main guérit.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Six fois il te délivrera de l’angoisse, Et sept fois le mal ne t’atteindra pas.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
Il te sauvera de la mort pendant la famine, Et des coups du glaive pendant la guerre.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Tu seras à l’abri du fléau de la langue, Tu seras sans crainte quand viendra la dévastation.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Tu te riras de la dévastation comme de la famine, Et tu n’auras pas à redouter les bêtes de la terre;
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Car tu feras alliance avec les pierres des champs, Et les bêtes de la terre seront en paix avec toi.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Tu jouiras du bonheur sous ta tente, Tu retrouveras tes troupeaux au complet,
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Tu verras ta postérité s’accroître, Et tes rejetons se multiplier comme l’herbe des champs.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Tu entreras au sépulcre dans la vieillesse, Comme on emporte une gerbe en son temps.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Voilà ce que nous avons reconnu, voilà ce qui est; A toi d’entendre et de mettre à profit.

< Ayubu 5 >