< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Appelle donc! Est-il quelqu’un qui te répondra? Vers lequel des Saints te tourneras-tu?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Certes, c’est sa mauvaise humeur qui tue l’insensé, c’est son dépit qui fait mourir le sot.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
J’Ai vu, moi, l’insensé prendre racine, mais aussitôt j’ai maudit sa demeure:
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
"Que ses fils soient éloignés de tout secours, qu’ils soient écrasés à la Porte, sans personne pour les sauver!
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Que l’affamé dévore sa récolte en l’enlevant jusque derrière les haies d’épines, que le besogneux happe ses richesses!"
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Car ce n’est pas du sol que sort le malheur, ce n’est pas de la terre que germe la douleur.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Mais l’homme est né pour la douleur, tout comme les étincelles enflammées s’élèvent haut dans l’air.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Toutefois, moi, je m’adresserais au Tout-Puissant, j’exposerais ma cause à Dieu.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Il accomplit de grandes choses en nombre infini, des merveilles qui ne peuvent se compter.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
II répand la pluie à la surface de la terre et lance des cours d’eaux dans les plaines.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Il met sur les hauteurs ceux qui étaient abaissés, et ceux qui étaient dans une noire tristesse se relèvent par son secours.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Il fait échouer les projets des gens de ruse: leurs mains n’exécutent rien qui vaille.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Il prend les malins dans leurs propres artifices et ruine les plans des fourbes.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Le jour, ils se heurtent aux ténèbres; en plein midi, ils tâtonnent comme dans la nuit.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
II protège contre leur bouche qui est un glaive, sauve le faible des mains du fort.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
L’Espoir renaît pour le pauvre, et l’iniquité a la bouche close.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Ah! Certes, heureux l’homme que Dieu réprimande! Ne repousse donc pas les leçons du Tout-Puissant.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Car il blesse et panse la blessure, il frappe et ses mains guérissent.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Qu’il survienne six calamités, il t’en préservera, et lors de la septième, le mal ne te touchera pas.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
En temps de famine, il te sauvera de la mort; dans le combat des atteintes du glaive.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Tu seras à l’abri du fouet de la langue, et si une catastrophe éclate, tu n’auras rien à craindre.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Tu te riras de la dévastation et de la disette; les animaux de la terre, tu ne les redouteras point.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Car même avec les pierres du sol tu auras un pacte, et les animaux sauvages concluront un traité de paix avec toi.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Tu verras le bonheur fixé dans ta demeure, tu inspecteras ta maison et ne trouveras rien en défaut.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Tu verras s’accroître le nombre de tes enfants, et tes rejetons se multiplier comme l’herbe de la terre.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Tu entreras dans la tombe au terme extrême de la vieillesse, comme s’élève une meule de blé dans la saison voulue.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Tel est le fruit de nos réflexions, telle est la vérité: accueille-la et prends-la à cœur.

< Ayubu 5 >