< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Appelle donc! Y aura-t-il quelqu'un qui te réponde? Vers lequel des saints te tourneras-tu?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
La colère tue l'insensé, et l'emportement fait mourir le fou.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
J'ai vu l'insensé étendre ses racines, et soudain j'ai maudit sa demeure.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Plus de salut pour ses fils; on les écrase à la porte, et personne ne les défend.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
L'homme affamé dévore sa moisson, il franchit la haie d'épines et l'emporte; l'homme altéré engloutit ses richesses.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Car le malheur ne sort pas de la poussière, et la souffrance ne germe pas du sol,
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
de telle sorte que l'homme naisse pour la peine, comme les fils de la foudre pour élever leur vol.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
A ta place, je me tournerais vers Dieu, c'est vers lui que je dirigerais ma prière.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Il fait des choses grandes, qu'on ne peut sonder; des prodiges qu'on ne saurait compter.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Il verse la pluie sur la terre, il envoie les eaux sur les campagnes,
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
il exalte ceux qui sont abaissés, et les affligés retrouvent le bonheur.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Il déjoue les projets des perfides, et leurs mains ne peuvent réaliser leurs complots.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Il prend les habiles dans leur propre ruse, et renverse les conseils des hommes astucieux.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Durant le jour, ils rencontrent les ténèbres; en plein midi, ils tâtonnent comme dans la nuit.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Dieu sauve le faible du glaive de leur langue, et de la main du puissant.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Alors l'espérance revient au malheureux; et l'iniquité ferme la bouche.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Heureux l'homme que Dieu châtie! Ne méprise donc pas la correction du Tout-Puissant.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
Car il fait la blessure, et il la bande; il frappe, et sa main guérit.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Six fois il te délivrera de l'angoisse, et, à la septième, le mal ne t'atteindra pas.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
Dans la famine, il te sauvera de la mort; dans le combat, des coups de l'épée.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Tu seras à l'abri du fouet de la langue, tu seras sans crainte quand viendra la dévastation.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Tu te riras de la dévastation et de la famine, tu ne redouteras pas les bêtes de la terre.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Car tu auras une alliance avec les pierres des champs, et les bêtes de la terre seront en paix avec toi.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Tu verras le bonheur régner sous ta tente; tu visiteras tes pâturages, et rien n'y manquera.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Tu verras ta postérité s'accroître, et tes rejetons se multiplier comme l'herbe des champs.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Tu entreras mûr dans le tombeau, comme une gerbe qu'on enlève en son temps.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Voilà ce que nous avons observé: c'est la vérité! Ecoute-le, et fais-en ton profit.

< Ayubu 5 >