< Ayubu 5 >
1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Pray, call, is there any to answer thee? And unto which of the holy ones dost thou turn?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
For provocation slayeth the perverse, And envy putteth to death the simple,
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
I — I have seen the perverse taking root, And I mark his habitation straightway,
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Far are his sons from safety, And they are bruised in the gate, And there is no deliverer.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Whose harvest the hungry doth eat, And even from the thorns taketh it, And the designing swallowed their wealth.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
For sorrow cometh not forth from the dust, Nor from the ground springeth up misery.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
For man to misery is born, And the sparks go high to fly.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Yet I — I inquire for God, And for God I give my word,
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Doing great things, and there is no searching. Wonderful, till there is no numbering.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Who is giving rain on the face of the land, And is sending waters on the out-places.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
To set the low on a high place, And the mourners have been high [in] safety.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Making void thoughts of the subtile, And their hands do not execute wisdom.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Capturing the wise in their subtilty, And the counsel of wrestling ones was hastened,
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
By day they meet darkness, And as night — they grope at noon.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
And He saveth the wasted from their mouth, And from a strong hand the needy,
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
And there is hope to the poor, And perverseness hath shut her mouth.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Lo, the happiness of mortal man, God doth reprove him: And the chastisement of the Mighty despise not,
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
For He doth pain, and He bindeth up, He smiteth, and His hands heal.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
In six distresses He delivereth thee, And in seven evil striketh not on thee.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
In famine He hath redeemed thee from death, And in battle from the hands of the sword.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
When the tongue scourgeth thou art hid, And thou art not afraid of destruction, When it cometh.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
At destruction and at hunger thou mockest, And of the beast of the earth, Thou art not afraid.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
(For with sons of the field [is] thy covenant, And the beast of the field Hath been at peace with thee.)
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
And thou hast known that thy tent [is] peace, And inspected thy habitation, and errest not,
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
And hast known that numerous [is] Thy seed, And thine offspring as the herb of the earth;
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Thou comest in full age unto the grave, As the going up of a stalk in its season.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Lo, this — we searched it out — it [is] right, hearken; And thou, know for thyself!