< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Therfor clepe thou, if `ony is that schal answere thee, and turne thou to summe of seyntis.
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Wrathfulnesse sleeth `a fonned man, and enuye sleeth a litil child.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
Y siy a fool with stidefast rote, and Y curside his feirnesse anoon.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Hise sones schulen be maad fer fro helthe, and thei schulen be defoulid in the yate, and `noon schal be that schal delyuere hem.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Whos ripe corn an hungri man schal ete, and an armed man schal rauysche hym, and thei, that thirsten, schulen drynke hise richessis.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
No thing is doon in erthe with out cause, and sorewe schal not go out of the erthe.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
A man is borun to labour, and a brid to fliyt.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Wherfor Y schal biseche the Lord, and Y schal sette my speche to my God.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
That makith grete thingis, and that moun not be souyt out, and wondurful thingis with out noumbre.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Which yyueth reyn on the face of erthe, and moistith alle thingis with watris.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Which settith meke men an hiy, and reisith with helthe hem that morenen.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Which distrieth the thouytis of yuel willid men, that her hondis moun not fille tho thingis that thei bigunnen.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Which takith cautelouse men in the felnesse `of hem, and distrieth the counsel of schrewis.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Bi dai thei schulen renne in to derknessis, and as in nyyt so thei schulen grope in myddai.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Certis God schal make saaf a nedi man fro the swerd of her mouth, and a pore man fro the hond of the violent, `ethir rauynour.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
And hope schal be to a nedi man, but wickidnesse schal drawe togidere his mouth.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Blessid is the man, which is chastisid of the Lord; therfor repreue thou not the blamyng of the Lord.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
For he woundith, and doith medicyn; he smytith, and hise hondis schulen make hool.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
In sixe tribulaciouns he schal delyuere thee, and in the seuenthe tribulacioun yuel schal not touche thee.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
In hungur he schal delyuere thee fro deeth, and in batel fro the power of swerd.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Thou schalt be hid fro the scourge of tunge, and thou schalt not drede myseiste, `ethir wretchidnesse, whanne it cometh.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
In distriyng maad of enemyes and in hungur thou schalt leiye, and thou schalt not drede the beestis of erthe.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
But thi couenaunt schal be with the stonys of erthe, and beestis of erthe schulen be pesible to thee.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
And thou schalt wite, that thi tabernacle hath pees, and thou visitynge thi fairnesse schalt not do synne.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
And thou schalt wite also, that thi seed schal be many fold, and thi generacioun schal be as an erbe of erthe.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
In abundaunce thou schalt go in to the sepulcre, as an heep of wheete is borun in his tyme.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Lo! this is so, as we han souyt; which thing herd, trete thou in minde.

< Ayubu 5 >