< Ayubu 5 >
1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Call, I pray thee—is there one to answer thee? Or, to which of the holy ones, wilt thou turn?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
For, to the foolish man, death is caused by vexation, and, the simple one, is slain by jealousy.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
I, have seen the foolish taking root, and then hath his home decayed, in a moment:
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
His children are far removed from safety, and they are crushed in the gate, and there is none to deliver:
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Whose harvest, the hungry, eateth up, and, even out of thorn hedges, he taketh it, and the snare gapeth for their substance.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
For sorrow, cometh not forth out of the dust, —nor, out of the ground, sprouteth trouble.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Though, man, to trouble, were born, as, sparks, on high, do soar,
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Yet indeed, I, would seek unto El, and, unto Elohim, would I set forth any cause: —
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Who doeth great things, beyond all search, —Wondrous things, till they cannot be recounted;
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Who giveth rain, upon the face of the earth, and sendeth forth waters, over the face of the open fields;
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Setting the lowly on high, and, mourners, are uplifted to safety;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Who doth frustrate the schemes of the crafty, that their hands cannot achieve abiding success;
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Who captureth the wise in their own craftiness, yea the headlong counsel of the crooked:
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
By day, they encounter darkness, and, as though it were night, they grope at high noon.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
But he saveth from the sword, out of their mouth, and, out of the hand of the strong, the needy.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Thus to the poor hath come hope, and, perversity, hath shut her mouth.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Lo! how happy is the man whom God correcteth! Therefore, the chastening of the Almighty, do not thou refuse;
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
For, he, woundeth that he may bind up, He smiteth through, that, his own hands, may heal.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
In six troubles, he will rescue thee, and, in seven, there shall smite thee no misfortune:
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
In famine, he will ransom thee from death, and in battle from the power of the sword;
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
During the scourge of the tongue, shalt thou be hid, neither shalt thou be afraid of destruction when it cometh;
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
At destruction and at hunger, shalt thou laugh, and, of the wild beast of the earth, be not thou afraid;
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
For, with the stones of the field, shall be thy covenant, and, the wild beast of the field, hath been made thy friend;
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
And thou shalt know that, at peace, is thy tent, and shalt visit thy fold, and miss nothing;
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
And thou shalt know, that numerous is thy seed, and, thine offspring, like the young shoots of the field.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Thou shalt come, yet robust, to the grave, as a stack of sheaves mounteth up in its season.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Lo! as for this, we have searched it out—so, it is, Hear it, and know, thou, for thyself.