< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Call now, see if any will answer thee! And to which of the holy ones wilt thou look?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Verily grief destroyeth the fool, And wrath consumeth the weak man.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
I have seen an impious man taking root, But soon I cursed his habitation.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
His children are far from safety; They are oppressed at the gate, and there is none to deliver them.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
His harvest the hungry devour, Carrying it even through the thorns; And a snare gapeth after his substance.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
For affliction cometh not from the dust, Nor doth trouble spring up from the ground;
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Behold, man is born to trouble, As the sparks fly upward.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
I would look to God, And to God would I commit my cause,
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Who doeth great things and unsearchable; Yea, marvellous things without number;
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
Who giveth rain upon the earth, And sendeth water upon the fields;
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Who placeth the lowly in high places, And restoreth the afflicted to prosperity;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
Who disappointeth the devices of the crafty, So that their hands cannot perform their enterprises;
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Who taketh the wise in their own craftiness, And bringeth to nought the counsel of the artful.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
They meet with darkness in the daytime; They grope at noon as if it were night.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
So he saveth the persecuted from their mouth; The oppressed from the hand of the mighty.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
So the poor hath hope, And iniquity stoppeth her mouth.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Behold, happy is the man whom God correcteth; Therefore despise not thou the chastening of the Almighty.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
For he bruiseth, and bindeth up; He woundeth, and his hands make whole.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
In six troubles will he deliver thee; Yea, in seven shall no evil touch thee.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
In famine he will redeem thee from death, And in war from the power of the sword.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Thou shalt be safe from the scourge of the tongue, And shalt not be afraid of destruction, when it cometh.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
At destruction and famine thou shalt laugh, And of the wild beasts of the land shalt thou not be afraid.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
For thou shalt be in league with the stones of the field; Yea, the beasts of the forest shall be at peace with thee.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
Thou shalt find that thy tent is in peace; Thou shalt visit thy dwelling, and not be disappointed.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Thou shalt see thy descendants numerous, And thine offspring as the grass of the earth.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Thou shalt come to thy grave in full age, As a shock of corn gathered in its season.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Lo! this we have searched out; so it is: Hear it, and lay it up in thy mind!

< Ayubu 5 >