< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Therefore call, if there are any who will respond to you, and turn to one or another of the saints.
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Truly, anger condemns the foolish to death, and envy kills the petty.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
I have seen a fool with a strong root, and I have cursed his excellence without hesitation.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
His sons will be far from prosperity and will be crushed at the gate, and there will be none who can rescue them.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Their harvest, the starving will eat. The armed man will rob him, and the thirsty will drink his resources.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Nothing on earth occurs without a reason, and sorrow does not rise from the earth.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
Man is born to labor, and the bird to fly.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Therefore, because of this, I will beg the Lord, and place my eloquence before God.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
He does great and unfathomable and miraculous things without number.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
He gives rain over the face of the earth and irrigates all things with the waters.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
He places the humble on high and encourages the grieving towards health.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
He dispels the thoughts of the spiteful, lest their hands be able to complete what they had begun.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
He catches the wise in their cleverness and dissipates the counsel of the perverse.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
They will encounter darkness in the daytime, and they will grope at midday just as in the night.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
Thereafter, he will act to save the needy from the sword of their mouth, and the poor from the hand of the violent.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
And there will be hope for those in need, for iniquity will diminish its speech.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Blessed is the man whom God corrects; therefore, do not reject the chastisement of the Lord.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
For he wounds and he cures; he strikes and his hands will heal.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
He will deliver you into six tribulations, and in the seventh, evil will not touch you.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
During famine, he will rescue you from death, and during war, from the hand of the sword.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
You will be hidden from the scourge of the tongue, and you will not fear calamity when it arrives.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
In desolation and in famine, you will laugh, and you will not dread the beasts of the earth.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
For you are in harmony with the stones of the land, and the beasts of the earth will make peace with you.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
And you will know that your home has peace, and, concerning your appearance, you will not sin.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Likewise, you will know that your offspring will be manifold and your progeny will be like the grass of the earth.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
You will enter the grave with abundance, just as a crop of wheat is gathered in its time.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Behold, this is just as we have found it, which you have heard; walk it through your mind.

< Ayubu 5 >