< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Call now, is there any who will answer thee? And to which of the holy ones will thou turn?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
For vexation kills the foolish man, and jealousy slays the silly one.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
I have seen the foolish taking root, but suddenly I cursed his habitation.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
His sons are far from safety, and they are crushed in the gate. Neither is there any to deliver them,
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
whose harvest the hungry eat up, and takes it even out of the thorns, and the snare gapes for their substance.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
For affliction does not come forth from the dust, nor does trouble spring out of the ground,
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
but man is born to trouble, as the sparks fly upward.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
But as for me, I would seek to God. And to God I would commit my cause,
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
who does great things and unsearchable, marvelous things without number,
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
who gives rain upon the earth, and sends waters upon the fields,
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
so that he sets up on high those who are low, and those who mourn are exalted to safety.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
He frustrates the devices of the crafty so that their hands cannot perform their enterprise.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
He takes the wise in their own craftiness, and the counsel of the cunning is carried headlong.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
They meet with darkness in the daytime, and grope at noonday as in the night.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
But he saves from the sword of their mouth, even the needy from the hand of the mighty.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
So a poor man has hope, and iniquity stops her mouth.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Behold, happy is the man whom God corrects. Therefore do not despise thou the chastening of the Almighty.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
For he injures, and binds up. He wounds, and his hands make whole.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
He will deliver thee in six troubles. Yea, in seven there shall no evil touch thee.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
In famine he will redeem thee from death, and in war from the power of the sword.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Thou shall be hid from the scourge of the tongue. Neither shall thou be afraid of destruction when it comes.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
At destruction and dearth thou shall laugh, nor shall thou be afraid of the beasts of the earth.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
For thou shall be in league with the stones of the field, and the beasts of the field shall be at peace with thee.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
And thou shall know that thy tent is in peace, and thou shall visit thy fold, and shall miss nothing.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Thou shall know also that thy seed shall be great, and thine offspring as the grass of the earth.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
Thou shall come to thy grave in a full age, like a shock of grain comes in its season.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Lo this, we have searched it, so it is. Hear it, and know thou it for thy good.

< Ayubu 5 >